< Ayubu 38 >

1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
ויען יהוה את איוב מן הסערה ויאמר׃
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
מי זה מחשיך עצה במלין בלי דעת׃
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
אזר נא כגבר חלציך ואשאלך והודיעני׃
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
איפה היית ביסדי ארץ הגד אם ידעת בינה׃
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
מי שם ממדיה כי תדע או מי נטה עליה קו׃
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
על מה אדניה הטבעו או מי ירה אבן פנתה׃
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
ברן יחד כוכבי בקר ויריעו כל בני אלהים׃
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
ויסך בדלתים ים בגיחו מרחם יצא׃
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
בשומי ענן לבשו וערפל חתלתו׃
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
ואשבר עליו חקי ואשים בריח ודלתים׃
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
ואמר עד פה תבוא ולא תסיף ופא ישית בגאון גליך׃
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
המימיך צוית בקר ידעתה שחר מקמו׃
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
לאחז בכנפות הארץ וינערו רשעים ממנה׃
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
תתהפך כחמר חותם ויתיצבו כמו לבוש׃
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
וימנע מרשעים אורם וזרוע רמה תשבר׃
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
הבאת עד נבכי ים ובחקר תהום התהלכת׃
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
הנגלו לך שערי מות ושערי צלמות תראה׃
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
התבננת עד רחבי ארץ הגד אם ידעת כלה׃
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
אי זה הדרך ישכן אור וחשך אי זה מקמו׃
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
כי תקחנו אל גבולו וכי תבין נתיבות ביתו׃
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
ידעת כי אז תולד ומספר ימיך רבים׃
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
הבאת אל אצרות שלג ואצרות ברד תראה׃
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
אשר חשכתי לעת צר ליום קרב ומלחמה׃
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
אי זה הדרך יחלק אור יפץ קדים עלי ארץ׃
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
מי פלג לשטף תעלה ודרך לחזיז קלות׃
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
להמטיר על ארץ לא איש מדבר לא אדם בו׃
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
להשביע שאה ומשאה ולהצמיח מצא דשא׃
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
היש למטר אב או מי הוליד אגלי טל׃
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
מבטן מי יצא הקרח וכפר שמים מי ילדו׃
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
כאבן מים יתחבאו ופני תהום יתלכדו׃
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
התקשר מעדנות כימה או משכות כסיל תפתח׃
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
התציא מזרות בעתו ועיש על בניה תנחם׃
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
הידעת חקות שמים אם תשים משטרו בארץ׃
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
התרים לעב קולך ושפעת מים תכסך׃
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
התשלח ברקים וילכו ויאמרו לך הננו׃
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
מי שת בטחות חכמה או מי נתן לשכוי בינה׃
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
מי יספר שחקים בחכמה ונבלי שמים מי ישכיב׃
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
בצקת עפר למוצק ורגבים ידבקו׃
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
התצוד ללביא טרף וחית כפירים תמלא׃
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
כי ישחו במעונות ישבו בסכה למו ארב׃
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
מי יכין לערב צידו כי ילדו אל אל ישועו יתעו לבלי אכל׃

< Ayubu 38 >