< Ayubu 38 >
1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
Konsa, Bondye te reponn Job nan van toubiyon an:
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
Se kilès sa a ki twouble konsèy Mwen an ak pawòl san konesans yo?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Alò, mare senti ou tankou gason, M ap mande ou e ou va enstwi M!
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
“Kote ou te ye lè M te poze fondasyon mond lan? Pale si ou gen bon konprann,
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
Se kilès ki te etabli mezi li? Konsi ou konnen? Oswa se kilès ki te lonje lign sou li?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
Sou kilès baz li yo te fonse? Oswa se kilès ki te poze ang prensipal li a,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
lè zetwal maten yo te chante ansanm, e tout fis Bondye yo te rele fò ak gran jwa?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
“Oswa se kilès ki te delimite lanmè a ak pòt yo, lè l te pete sòti nan vant lemonn nan;
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
lè M te fè yon nwaj sèvi vètman li e fènwa byen pwès kon rad anfans li,
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
epi Mwen te plase lizyè sou li, e te kadnase pòt li yo,
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
lè Mwen te di: ‘Men la, ou va rive e pa plis; men la vag ògèy ou va rete’?
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
“Èske pandan tout vi ou, ou te pase lòd pou maten rive, e fè solèy granmaten an konnen plas li,
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
pou l ta kenbe mechan yo sou pwent latè e souke l nèt pou yo sòti ladann?
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
Li vin chanje tankou ajil anba yon so; epi prezante la tankou yon abiman.
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
Sou mechan yo, limyè yo retire e bwa souleve a vin kase.
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
“Èske ou konn antre nan sous lanmè yo, oswa mache nan fon pwofondè a?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
Èske pòtay lanmò yo te konn vin vizib a ou menm? Oswa èske ou konn wè pòtay lonbraj lanmò yo?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
Èske ou te konprann gwosè ak lajè tout tè a? Di M si ou konnen tout sa a.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
“Kote chemen an ye pou rive nan abitasyon limyè a? Epi tenèb la, kote landwa li,
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
pou ou ta mennen li nan limit li, pou ou ta kab konprann chemen pou rive lakay li?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Fòk ou konnen paske ou te fèt avan sa, e kantite jou ou yo vast!
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
Èske ou konn antre nan kay depo nèj yo, oswa èske ou konn wè kay depo pou lagrèl yo,
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
ke M te rezève pou tan twoub la, pou jou lagè ak batay la?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
Kote chemen a ki pou fè loray divize a oswa ki kote van lès la te gaye sou tè a?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
“Se kilès ki te kreve yon kanal pou gran inondasyon an, oswa yon chemen pou eklè ak tonnè a,
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
Pou mennen lapli nan yon teren kote nanpwen moun, nan yon dezè san pèsòn ladann,
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
Pou satisfè yon peyi savann dezole e fè grenn zèb yo vin jèmen.
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
Èske lapli gen papa? Oswa se kilès ki te reyisi fè gout lawouze yo?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
Nan ki vant manman a sila glas la te sòti? Epi fredi syèl la, se kilès ki te fè nesans li?
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
Dlo vin di tankou wòch e sifas pwofondè a vin prizonye ladann.
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
“Èske ou konn mare chenn zetwal Pleiades yo, oswa lage kòd zetwal Orion yo?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
Èske ou kab mennen fè parèt tout sign Zodyak yo nan sezon yo, oswa gide zetwal Gran Lous la ak pitit li yo?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
Èske ou konnen tout règleman syèl la, oswa èske ou kab etabli règleman pa yo sou tè a?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
Èske ou kab leve vwa ou rive nan nwaj yo, pou fè gwo kantite dlo vin kouvri ou?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
Èske ou kab voye ekleraj yo pou yo rive di ou: ‘Men nou isit la’?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
Se kilès ki te mete sajès nan kè lòm, oswa te bay bon konprann nan panse a?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
Se kilès ki kab konte nwaj yo ak sajès, oswa vide gwo krich dlo syèl yo,
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
Pou pousyè a vin di nan yon gwo ma dlo e bòl tè yo vin kole ansanm?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
“Èske ou kab fè lachas pou bay lyon an manje, oswa satisfè apeti a jenn ti lyon yo,
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
Lè yo kouche nan kav pa yo e kouche tann pèlen bò lakay yo?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Se kilès ki prepare manje pou kòbo a lè pitit li rele kote Bondye e mache gaye grangou?