< Ayubu 38 >
1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
L’Éternel répondit à Job du milieu de la tempête et dit:
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
Qui est celui qui obscurcit mes desseins Par des discours sans intelligence?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Ceins tes reins comme un vaillant homme; Je t’interrogerai, et tu m’instruiras.
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
Où étais-tu quand je fondais la terre? Dis-le, si tu as de l’intelligence.
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
Qui en a fixé les dimensions, le sais-tu? Ou qui a étendu sur elle le cordeau?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
Sur quoi ses bases sont-elles appuyées? Ou qui en a posé la pierre angulaire,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
Alors que les étoiles du matin éclataient en chants d’allégresse, Et que tous les fils de Dieu poussaient des cris de joie?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
Qui a fermé la mer avec des portes, Quand elle s’élança du sein maternel;
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
Quand je fis de la nuée son vêtement, Et de l’obscurité ses langes;
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
Quand je lui imposai ma loi, Et que je lui mis des barrières et des portes;
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
Quand je dis: Tu viendras jusqu’ici, tu n’iras pas au-delà; Ici s’arrêtera l’orgueil de tes flots?
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
Depuis que tu existes, as-tu commandé au matin? As-tu montré sa place à l’aurore,
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
Pour qu’elle saisisse les extrémités de la terre, Et que les méchants en soient secoués;
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
Pour que la terre se transforme comme l’argile qui reçoit une empreinte, Et qu’elle soit parée comme d’un vêtement;
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
Pour que les méchants soient privés de leur lumière, Et que le bras qui se lève soit brisé?
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
As-tu pénétré jusqu’aux sources de la mer? T’es-tu promené dans les profondeurs de l’abîme?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
Les portes de la mort t’ont-elles été ouvertes? As-tu vu les portes de l’ombre de la mort?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
As-tu embrassé du regard l’étendue de la terre? Parle, si tu sais toutes ces choses.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
Où est le chemin qui conduit au séjour de la lumière? Et les ténèbres, où ont-elles leur demeure?
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
Peux-tu les saisir à leur limite, Et connaître les sentiers de leur habitation?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Tu le sais, car alors tu étais né, Et le nombre de tes jours est grand!
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
Es-tu parvenu jusqu’aux amas de neige? As-tu vu les dépôts de grêle,
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
Que je tiens en réserve pour les temps de détresse, Pour les jours de guerre et de bataille?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
Par quel chemin la lumière se divise-t-elle, Et le vent d’orient se répand-il sur la terre?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
Qui a ouvert un passage à la pluie, Et tracé la route de l’éclair et du tonnerre,
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
Pour que la pluie tombe sur une terre sans habitants, Sur un désert où il n’y a point d’hommes;
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
Pour qu’elle abreuve les lieux solitaires et arides, Et qu’elle fasse germer et sortir l’herbe?
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
La pluie a-t-elle un père? Qui fait naître les gouttes de la rosée?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
Du sein de qui sort la glace, Et qui enfante le frimas du ciel,
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
Pour que les eaux se cachent comme une pierre, Et que la surface de l’abîme soit enchaînée?
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
Noues-tu les liens des Pléiades, Ou détaches-tu les cordages de l’Orion?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
Fais-tu paraître en leur temps les signes du zodiaque, Et conduis-tu la Grande Ourse avec ses petits?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
Connais-tu les lois du ciel? Règles-tu son pouvoir sur la terre?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
Élèves-tu la voix jusqu’aux nuées, Pour appeler à toi des torrents d’eaux?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
Lances-tu les éclairs? Partent-ils? Te disent-ils: Nous voici?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
Qui a mis la sagesse dans le cœur, Ou qui a donné l’intelligence à l’esprit?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
Qui peut avec sagesse compter les nuages, Et verser les outres des cieux,
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
Pour que la poussière se mette à ruisseler, Et que les mottes de terre se collent ensemble?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
Chasses-tu la proie pour la lionne, Et apaises-tu la faim des lionceaux,
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
Quand ils sont couchés dans leur tanière, Quand ils sont en embuscade dans leur repaire?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Qui prépare au corbeau sa pâture, Quand ses petits crient vers Dieu, Quand ils sont errants et affamés?