< Ayubu 38 >
1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
Alors Yahweh répondit à Job du sein de la tempête, et dit:
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
Quel est celui qui obscurcit ainsi le plan divin, par des discours sans intelligence?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Ceins tes reins, comme un homme: je vais t’interroger, et tu m’instruiras.
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
Où étais-tu quand je posais les fondements de la terre? Dis-le, si tu as l’intelligence.
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
Qui en a fixé les dimensions? Le sais-tu? Qui a tendu sur elle le cordeau?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
Sur quoi ses bases reposent-elles, ou qui en a posé la pierre angulaire,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
quand les astres du matin chantaient en chœur, et que tous les fils de Dieu poussaient des cris d’allégresse?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
Qui a fermé la mer avec des portes, lorsqu’elle sortit impétueuse du sein maternel;
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
quand je lui donnai les nuages pour vêtements, et pour langes d’épais brouillards;
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
quand je lui imposai ma loi, que je lui mis des portes et des verrous,
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
et que je lui dis: « Tu viendras jusqu’ici, non au delà; ici s’arrêtera l’orgueil de tes flots »?
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
As-tu, depuis que tu existes, commandé au matin? As-tu indiqué sa place à l’aurore,
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
pour qu’elle saisisse les extrémités de la terre et qu’elle en secoue les méchants;
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
pour que la terre prenne forme, comme l’argile sous le cachet, et qu’elle se montre parée comme d’un vêtement;
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
pour que les malfaiteurs soient privés de leur lumière, et que le bras levé pour le crime soit brisé?
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
Es-tu descendu jusqu’aux sources de la mer, t’es-tu promené dans les profondeurs de l’abîme?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
Les portes de la mort se sont-elles ouvertes devant toi, as-tu vu les portes du sombre séjour?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
As-tu embrassé l’étendue de la terre? Parle, si tu sais toutes ces choses.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
Où est le chemin qui conduit au séjour de la lumière, et où se trouve la demeure des ténèbres?
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
Tu pourrais les saisir en leur domaine, tu connais les sentiers de leur séjour!…
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Tu le sais sans doute, puisque tu étais né avant elles; le nombre de tes jours est si grand!…
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
Es-tu entré dans les trésors de la neige? As-tu vu les réservoirs de la grêle,
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
que je tiens prêts pour le temps de la détresse, pour les jours de la guerre et du combat?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
Par quelle voie la lumière se divise-t-elle, et le vent d’orient se répand-il sur la terre?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
Qui a ouvert des canaux aux ondées, et tracé une route aux feux du tonnerre,
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
afin que la pluie tombe sur une terre inhabitée, sur le désert où il n’y a point d’hommes;
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
pour qu’elle arrose la plaine vaste et vide, et y fasse germer l’herbe verte!
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
La pluie a-t-elle un père? Qui engendre les gouttes de la rosée?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
De quel sein sort la glace? Et le givre du ciel, qui l’enfante,
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
pour que les eaux durcissent comme la pierre, et que la surface de l’abîme se solidifie?
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
Est-ce toi qui serres les liens des Pléiades, ou pourrais-tu relâcher les chaînes d’Orion?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
Est-ce toi qui fais lever les constellations en leur temps, qui conduis l’Ourse avec ses petits?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
Connais-tu les lois du ciel, règles-tu ses influences sur la terre?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
Élèves-tu ta voix jusque dans les nues, pour que des torrents d’eau tombent sur toi?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
Est-ce toi qui lâches les éclairs pour qu’ils partent, et te disent-ils: « Nous voici! »
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
Qui a mis la sagesse dans les nuées, ou qui a donné l’intelligence aux météores?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
Qui peut exactement compter les nuées, incliner les urnes du ciel,
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
pour que la poussière se forme en masse solide et que les glèbes adhèrent ensemble?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
Est-ce toi qui chasses pour la lionne sa proie, qui rassasies la faim des lionceaux,
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
quand ils sont couchés dans leur tanière, qu’ils se tiennent en embuscade dans le taillis?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Qui prépare au corbeau sa pâture, quand ses petits crient vers Dieu, qu’ils errent çà et là, sans nourriture?