< Ayubu 38 >
1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
Et Yahvé répondit à Job du haut du tourbillon,
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
« Qui est celui qui obscurcit le conseil par des mots sans connaissance?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Accrochez-vous comme un homme, car je t'interrogerai, puis tu me répondras!
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
« Où étiez-vous lorsque j'ai posé les fondations de la terre? Déclarez, si vous avez de la compréhension.
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
Qui a déterminé ses mesures, si vous le savez? Ou qui a dépassé les bornes?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
Sur quoi ses fondations étaient-elles fixées? Ou qui a posé sa pierre angulaire,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
quand les étoiles du matin chantaient ensemble, et tous les fils de Dieu ont crié de joie?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
« Ou qui a fermé la mer avec des portes, quand il est sorti de l'utérus,
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
quand j'ai fait des nuages son vêtement, et l'a enveloppé dans une épaisse obscurité,
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
marqués pour cela ma limite, fixer les barres et les portes,
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
et dit: « Vous pouvez venir ici, mais pas plus loin. Vos fières vagues seront arrêtées ici »?
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
« De ton temps, tu as donné des ordres au matin, et a permis à l'aube de connaître sa place,
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
pour s'emparer des extrémités de la terre, et en faire sortir les méchants?
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
Il est changé comme l'argile sous le sceau, et présenté comme un vêtement.
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
La lumière est cachée aux méchants. Le bras supérieur est cassé.
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
« Es-tu entré dans les sources de la mer? Ou avez-vous marché dans les recoins des profondeurs?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
Les portes de la mort se sont-elles révélées à vous? Ou avez-vous vu les portes de l'ombre de la mort?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
As-tu compris la terre dans sa largeur? Déclarez, si vous savez tout.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
« Quel est le chemin vers la demeure de la lumière? Quant à l'obscurité, où est sa place,
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
que vous devez le prendre à sa limite, pour que tu discernes les chemins de sa maison?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Tu le sais certainement, car tu es né à cette époque, et le nombre de vos jours est grand!
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
Vous êtes entrés dans les entrepôts de la neige, ou avez-vous vu les entrepôts de la grêle,
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
que j'ai réservé pour le temps de la détresse, contre le jour de la bataille et de la guerre?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
De quelle manière la foudre est-elle distribuée, ou le vent d'est dispersé sur la terre?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
Qui a creusé un canal pour les eaux de crue, ou la trajectoire de l'orage,
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
pour faire pleuvoir sur un pays où il n'y a pas d'homme, dans le désert, où il n'y a pas d'homme,
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
pour rassasier le terrain vague et désolé, pour faire pousser l'herbe tendre?
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
La pluie a-t-elle un père? Ou qui est le père des gouttes de rosée?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
De quel ventre la glace est-elle sortie? Qui a donné naissance à la gelée grise du ciel?
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
Les eaux deviennent dures comme la pierre, lorsque la surface des profondeurs est gelée.
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
« Pouvez-vous lier l'amas des Pléiades, ou détacher les cordes d'Orion?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
Peux-tu diriger les constellations dans leur saison? Ou pouvez-vous guider l'ourse avec ses oursons?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
Connais-tu les lois des cieux? Pouvez-vous établir sa domination sur la terre?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
« Pouvez-vous élever votre voix vers les nuages, pour que l'abondance des eaux te couvre?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
Peux-tu envoyer des éclairs, pour qu'ils partent? Est-ce qu'ils vous disent: « Nous y voilà »?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
Qui a mis la sagesse dans les parties intérieures? Ou qui a donné de l'intelligence à l'esprit?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
Qui peut compter les nuages par la sagesse? Ou qui peut verser les récipients du ciel,
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
quand la poussière se transforme en masse, et les mottes de terre collent ensemble?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
« Peux-tu chasser la proie pour la lionne, ou satisfaire l'appétit des jeunes lions,
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
quand ils sont accroupis dans leur tanière, et se mettre à l'affût dans les fourrés?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Qui fournit au corbeau sa proie, quand ses petits crient vers Dieu, et errent par manque de nourriture?