< Ayubu 38 >

1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
Then the LORD answered Job out of the whirlwind, and said,
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
Who is this that darkens counsel by words without knowledge?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Gird up now your loins like a man; for I will demand of you, and answer you me.
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
Where were you when I laid the foundations of the earth? declare, if you have understanding.
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
Who has laid the measures thereof, if you know? or who has stretched the line on it?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
Whereupon are the foundations thereof fastened? or who laid the corner stone thereof;
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
When the morning stars sang together, and all the sons of God shouted for joy?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
Or who shut up the sea with doors, when it broke forth, as if it had issued out of the womb?
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
When I made the cloud the garment thereof, and thick darkness a swaddling cloth for it,
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
And broke up for it my decreed place, and set bars and doors,
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
And said, Till now shall you come, but no further: and here shall your proud waves be stayed?
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
Have you commanded the morning since your days; and caused the dayspring to know his place;
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
That it might take hold of the ends of the earth, that the wicked might be shaken out of it?
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
It is turned as clay to the seal; and they stand as a garment.
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
And from the wicked their light is withheld, and the high arm shall be broken.
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
Have you entered into the springs of the sea? or have you walked in the search of the depth?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
Have the gates of death been opened to you? or have you seen the doors of the shadow of death?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
Have you perceived the breadth of the earth? declare if you know it all.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
Where is the way where light dwells? and as for darkness, where is the place thereof,
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
That you should take it to the bound thereof, and that you should know the paths to the house thereof?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Know you it, because you were then born? or because the number of your days is great?
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
Have you entered into the treasures of the snow? or have you seen the treasures of the hail,
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
Which I have reserved against the time of trouble, against the day of battle and war?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
By what way is the light parted, which scatters the east wind on the earth?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
Who has divided a watercourse for the overflowing of waters, or a way for the lightning of thunder;
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
To cause it to rain on the earth, where no man is; on the wilderness, wherein there is no man;
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
To satisfy the desolate and waste ground; and to cause the bud of the tender herb to spring forth?
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
Has the rain a father? or who has begotten the drops of dew?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
Out of whose womb came the ice? and the hoary frost of heaven, who has gendered it?
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
The waters are hid as with a stone, and the face of the deep is frozen.
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
Can you bind the sweet influences of Pleiades, or loose the bands of Orion?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
Can you bring forth Mazzaroth in his season? or can you guide Arcturus with his sons?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
Know you the ordinances of heaven? can you set the dominion thereof in the earth?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
Can you lift up your voice to the clouds, that abundance of waters may cover you?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
Can you send lightning, that they may go and say to you, Here we are?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
Who has put wisdom in the inward parts? or who has given understanding to the heart?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
Who can number the clouds in wisdom? or who can stay the bottles of heaven,
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
When the dust grows into hardness, and the clods stuck fast together?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
Will you hunt the prey for the lion? or fill the appetite of the young lions,
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
When they couch in their dens, and abide in the covert to lie in wait?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Who provides for the raven his food? when his young ones cry to God, they wander for lack of meat.

< Ayubu 38 >