< Ayubu 38 >
1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
And Jehovah answered Job out of the whirlwind and said,
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
Who is this that darkeneth counsel by words without knowledge?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Gird up now thy loins like a man; and I will demand of thee, and inform thou me.
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
Where wast thou when I founded the earth? Declare, if thou hast understanding.
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
Who set the measures thereof — if thou knowest? or who stretched a line upon it?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
Whereupon were the foundations thereof sunken? or who laid its corner-stone,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
When the morning stars sang together, and all the sons of God shouted for joy?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
And who shut up the sea with doors, when it burst forth, issuing out of the womb?
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
When I made the cloud its garment, and thick darkness a swaddling band for it;
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
When I cut out for it my boundary, and set bars and doors,
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
And said, Hitherto shalt thou come and no further, and here shall thy proud waves be stayed?
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
Hast thou since thy days commanded the morning? hast thou caused the dawn to know its place,
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
That it might take hold of the ends of the earth, and the wicked might be shaken out of it?
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
It is changed like the signet-clay; and [all things] stand forth as in a garment:
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
And from the wicked their light is withholden, and the uplifted arm is broken.
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
Hast thou entered as far as the springs of the sea? and hast thou walked in the recesses of the deep?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
Have the gates of death been revealed unto thee? and hast thou seen the gates of the shadow of death?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
Hath thine understanding compassed the breadths of the earth? Declare if thou knowest it all.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
Where is the way to where light dwelleth? and the darkness, where is its place,
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
That thou shouldest take it to its bound, and that thou shouldest know the paths to its house?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Thou knowest, for thou wast then born, and the number of thy days is great!
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
Hast thou entered into the storehouses of the snow, and hast thou seen the treasuries of the hail,
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
Which I have reserved for the time of distress, for the day of battle and war?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
By what way is the light parted, [and] the east wind scattered upon the earth?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
Who hath divided a channel for the rain-flood, and a way for the thunder's flash;
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
To cause it to rain on the earth, where no one is; on the wilderness wherein there is not a man;
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
To satisfy the desolate and waste [ground], and to cause the sprout of the grass to spring forth?
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
Hath the rain a father? or who begetteth the drops of dew?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
Out of whose womb cometh the ice? and the hoary frost of heaven, who bringeth it forth?
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
When the waters lie hidden as in stone, and the face of the deep holdeth fast together.
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
Canst thou fasten the bands of the Pleiades, or loosen the cords of Orion?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
Dost thou bring forth the constellations each in its season? or dost thou guide the Bear with her sons?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
Knowest thou the ordinances of the heavens? dost thou determine their rule over the earth?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
Dost thou lift up thy voice to the clouds, that floods of waters may cover thee?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
Dost thou send forth lightnings that they may go, and say unto thee, Here we are?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
Who hath put wisdom in the inward parts? or who hath given understanding to the mind?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
Who numbereth the clouds with wisdom? or who poureth out the bottles of the heavens,
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
When the dust runneth as into a molten mass, and the clods cleave fast together?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
Dost thou hunt the prey for the lioness, and dost thou satisfy the appetite of the young lions,
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
When they crouch in [their] dens, [and] abide in the thicket to lie in wait?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Who provideth for the raven his food, when his young ones cry unto God, [and] they wander for lack of meat?