< Ayubu 37 >
1 Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
super hoc expavit cor meum et emotum est de loco suo
2 Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
audite auditionem in terrore vocis eius et sonum de ore illius procedentem
3 Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
subter omnes caelos ipse considerat et lumen illius super terminos terrae
4 Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
post eum rugiet sonitus tonabit voce magnitudinis suae et non investigabitur cum audita fuerit vox eius
5 Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
tonabit Deus in voce sua mirabiliter qui facit magna et inscrutabilia
6 Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
qui praecipit nivi ut descendat in terram et hiemis pluviis et imbri fortitudinis suae
7 Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
qui in manu omnium hominum signat ut noverint singuli opera sua
8 Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
ingredietur bestia latibulum et in antro suo morabitur
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
ab interioribus egreditur tempestas et ab Arcturo frigus
10 Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
flante Deo concrescit gelu et rursum latissimae funduntur aquae
11 Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
frumentum desiderat nubes et nubes spargunt lumen suum
12 Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
quae lustrant per circuitum quocumque eas voluntas gubernantis duxerit ad omne quod praeceperit illis super faciem orbis terrarum
13 Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
sive in una tribu sive in terra sua sive in quocumque loco misericordiae suae eas iusserit inveniri
14 Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
ausculta haec Iob sta et considera miracula Dei
15 Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
numquid scis quando praeceperit Deus pluviis ut ostenderent lucem nubium eius
16 Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
numquid nosti semitas nubium magnas et perfectas scientias
17 Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
nonne vestimenta tua calida sunt cum perflata fuerit terra austro
18 Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
tu forsitan cum eo fabricatus es caelos qui solidissimi quasi aere fusi sunt
19 Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
ostende nobis quid dicamus illi nos quippe involvimur tenebris
20 Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
quis narrabit ei quae loquor etiam si locutus fuerit homo devorabitur
21 Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
at nunc non vident lucem subito aer cogitur in nubes et ventus transiens fugabit eas
22 Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
ab aquilone aurum venit et ad Deum formidolosa laudatio
23 Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
digne eum invenire non possumus magnus fortitudine et iudicio et iustitia et enarrari non potest
24 Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”
ideo timebunt eum viri et non audebunt contemplari omnes qui sibi videntur esse sapientes