< Ayubu 37 >

1 Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
“Yes, at this my heart trembles, and is moved out of its place.
2 Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
Hear, oh, hear the noise of his voice, the sound that goes out of his mouth.
3 Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
He sends it out under the whole sky, and his lightning to the ends of the earth.
4 Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
After it a voice roars. He thunders with the voice of his majesty. He doesn’t hold back anything when his voice is heard.
5 Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
God thunders marvellously with his voice. He does great things, which we can’t comprehend.
6 Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
For he says to the snow, ‘Fall on the earth,’ likewise to the shower of rain, and to the showers of his mighty rain.
7 Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
He seals up the hand of every man, that all men whom he has made may know it.
8 Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
Then the animals take cover, and remain in their dens.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
Out of its room comes the storm, and cold out of the north.
10 Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
By the breath of God, ice is given, and the width of the waters is frozen.
11 Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
Yes, he loads the thick cloud with moisture. He spreads abroad the cloud of his lightning.
12 Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
It is turned around by his guidance, that they may do whatever he commands them on the surface of the habitable world,
13 Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
whether it is for correction, or for his land, or for loving kindness, that he causes it to come.
14 Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
“Listen to this, Job. Stand still, and consider the wondrous works of God.
15 Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
Do you know how God controls them, and causes the lightning of his cloud to shine?
16 Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
Do you know the workings of the clouds, the wondrous works of him who is perfect in knowledge?
17 Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
You whose clothing is warm when the earth is still by reason of the south wind?
18 Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
Can you, with him, spread out the sky, which is strong as a cast metal mirror?
19 Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
Teach us what we will tell him, for we can’t make our case by reason of darkness.
20 Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
Will it be told him that I would speak? Or should a man wish that he were swallowed up?
21 Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
Now men don’t see the light which is bright in the skies, but the wind passes, and clears them.
22 Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
Out of the north comes golden splendour. With God is awesome majesty.
23 Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
We can’t reach the Almighty. He is exalted in power. In justice and great righteousness, he will not oppress.
24 Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”
Therefore men revere him. He doesn’t regard any who are wise of heart.”

< Ayubu 37 >