< Ayubu 37 >

1 Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
At this my heart trembleth, And leapeth out of its place.
2 Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
Hear, O hear, the thunder of his voice, And the noise which goeth forth from his mouth!
3 Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
He directeth it under the whole heaven, And his lightning to the ends of the earth.
4 Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
After it the thunder roareth; He thundereth with his voice of majesty, And restraineth it not, when his voice is heard.
5 Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
God thundereth with his voice marvellously; Great things doeth he, which we cannot comprehend.
6 Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
For he saith to the snow, “Be thou on the earth!” To the shower also, even the showers of his might.
7 Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
He sealeth up the hand of every man, That all men whom he hath made may acknowledge him.
8 Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
Then the beasts go into dens, And abide in their caverns.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
Out of the south cometh the whirlwind, And cold out of the north.
10 Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
By the breath of God ice is formed, And the broad waters become narrow,
11 Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
Yea, with moisture he burdeneth the clouds; He spreadeth abroad his lightning-clouds.
12 Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
They move about by his direction, To execute all his commands throughout the world;
13 Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
Whether he cause them to come for punishment, Or for the land, or for mercy.
14 Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
Give ear to this, O Job! Stand still, and consider the wondrous works of God!
15 Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
Dost thou know when God gave commandment to them, And caused the lightning of his cloud to flash?
16 Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
Dost thou understand the balancing of the clouds, The wondrous works of Him that is perfect in knowledge?
17 Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
How thy garments become warm, When he maketh the earth still by the south wind?
18 Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
Canst thou like him spread out the sky, Which is firm like a molten mirror?
19 Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
Teach us what we shall say to him! For we cannot set in order our words by reason of darkness.
20 Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
Shall it be told him that I would speak? Shall a man speak, that he may be consumed?
21 Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
For now men do not look upon the light, When it is bright in the skies, When the wind hath passed over them, and made them clear.
22 Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
From the north cometh gold; But with God is terrible majesty!
23 Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
The Almighty, we cannot find him out; Great is he in power and justice, Abundant in righteousness; he doth not oppress.
24 Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”
Therefore let men fear him! Upon none of the wise in heart will he look.

< Ayubu 37 >