< Ayubu 37 >
1 Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
At this also my heart is troubled, and moved out of its place.
2 Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
Hear you a report by the anger of the Lord's wrath, and a discourse shall come out of his mouth.
3 Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
His dominion is under the whole heaven, and his light is at the extremities of the earth.
4 Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
After him shall be a cry with a [loud] voice; he shall thunder with the voice of his excellency, yet he shall not cause men to pass away, for one shall hear his voice.
5 Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
The Mighty One shall thunder wonderfully with his voice: for he has done great things which we knew not;
6 Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
commanding the snow, Be you upon the earth, and the stormy rain, and the storm of the showers of his might.
7 Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
He seals up the hand of every man, that every man may know his own weakness.
8 Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
And the wild beasts come in under the covert, and rest in [their] lair.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
Troubles come on out of the secret chambers, and cold from the mountain-tops.
10 Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
And from the breath of the Mighty One he will send frost; and he guides the water in whatever way he pleases.
11 Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
And [if] a cloud obscures [what is] precious [to him], his light will disperse the cloud.
12 Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
And he will carry round the encircling [clouds] by his governance, to [perform] their works: whatever he shall command them,
13 Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
this has been appointed by him on the earth, whether for correction, [or] for his land, or if he shall find him [an object] for mercy.
14 Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
Listen to this, O Job: stand still, and be admonished of the power of the Lord.
15 Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
We know that god has disposed his works, having made light out of darkness.
16 Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
And he knows the divisions of the clouds, and the signal overthrows of the ungodly.
17 Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
But your robe is warm, and there is quiet upon the land.
18 Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
Will you establish with him [foundations] for the ancient [heavens? they are] strong as a molten mirror.
19 Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
Therefore teach me, what shall we say to him? and let us cease from saying much.
20 Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
Have I a book or a scribe my me, that I may stand and put man to silence?
21 Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
But the light is not visible to all: it shines afar off in the heavens, as that which is from him in the clouds.
22 Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
From the [north] come the clouds shining like gold: in these great are the glory and honor of the Almighty;
23 Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
and we do not find another his equal in strength: [as for] him that judges justly, do you not think that he listens?
24 Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”
Therefore men shall fear him; and the wise also in heart shall fear him.