< Ayubu 37 >

1 Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
At this my heart trembleth, and is moved out of its place.
2 Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
Hear ye attentively the terror of his voice, and the sound that cometh out of his mouth.
3 Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
He beholdeth under all the heavens, and his light is upon the ends of the earth.
4 Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
After it a noise shall roar, he shall thunder with the voice of his majesty, and shall not be found out, when his voice shall be heard.
5 Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
God shall thunder wonderfully with his voice, he that doth great and unsearchable things.
6 Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
He commandeth the snow to go down upon the earth, and the winter rain, and the shower of his strength.
7 Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
He sealeth up the hand of all men, that every one may know his works.
8 Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
Then the beast shall go into his covert, and shall abide in his den.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
Out of the inner parts shall a tempest come, and cold out of the north.
10 Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
When God bloweth there cometh frost, and again the waters are poured out abundantly.
11 Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
Corn desireth clouds, and the clouds spread their light:
12 Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
Which go round about, whithersoever the will of him that governeth them shall lead them, to whatsoever he shall command them upon the face of the whole earth:
13 Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
Whether in one tribe, or in his own land, or in what place soever of his mercy he shall command them to be found.
14 Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
Hearken to these things, Job: Stand, and consider the wondrous works of God.
15 Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
Dost thou know when God commanded the rains, to shew his light of his clouds?
16 Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
Knowest thou the great paths of the clouds, and the perfect knowledges?
17 Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
Are not thy garments hot, when the south wind blows upon the earth?
18 Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
Thou perhaps hast made the heavens with him, which are most strong, as if they were of molten brass.
19 Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
Shew us what we may say to him: for we are wrapped up in darkness.
20 Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
Who shall tell him the things I speak? even if a man shall speak, he shall be swallowed up.
21 Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
But now they see not the light: the air on a sudden shall be thickened into clouds, and the wind shall pass and drive them away.
22 Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
Cold cometh out of the north, and to God praise with fear.
23 Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
We cannot find him worthily: he is great in strength, and in judgment, and in justice, and he is ineffable.
24 Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”
Therefore men shall fear him, and all that seem to themselves to be wise, shall not dare to behold him.

< Ayubu 37 >