< Ayubu 37 >
1 Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
At this my heart is shaking; it is moved out of its place.
2 Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
Give ear to the rolling noise of his voice; to the hollow sound which goes out of his mouth.
3 Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
He sends it out through all the heaven, and his thunder-flame to the ends of the earth.
4 Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
After it a voice is sounding, thundering out the word of his power; he does not keep back his thunder-flames; from his mouth his voice is sounding.
5 Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
He does wonders, more than may be searched out; great things of which we have no knowledge;
6 Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
For he says to the snow, Make the earth wet; and to the rain-storm, Come down.
7 Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
He puts an end to the work of every man, so that all may see his work.
8 Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
Then the beasts go into their holes, and take their rest.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
Out of its place comes the storm-wind, and the cold out of its store-houses.
10 Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
By the breath of God ice is made, and the wide waters are shut in.
11 Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
The thick cloud is weighted with thunder-flame, and the cloud sends out its light;
12 Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
And it goes this way and that, round about, turning itself by his guiding, to do whatever he gives orders to be done, on the face of his world of men,
13 Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
For a rod, or for a curse, or for mercy, causing it to come on the mark.
14 Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
Give ear to this, O Job, and keep quiet in your place; and take note of the wonders worked by God.
15 Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
Have you knowledge of God's ordering of his works, how he makes the light of his cloud to be seen?
16 Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
Have you knowledge of the balancings of the clouds, the wonders of him who has all wisdom?
17 Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
You, whose clothing is warm, when the earth is quiet because of the south wind,
18 Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
Will you, with him, make the skies smooth, and strong as a polished looking-glass?
19 Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
Make clear to me what we are to say to him; we are unable to put our cause before him, because of the dark.
20 Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
How may he have knowledge of my desire for talk with him? or did any man ever say, May destruction come on me?
21 Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
And now the light is not seen, for it is dark because of the clouds; but a wind comes, clearing them away.
22 Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
A bright light comes out of the north; God's glory is greatly to be feared.
23 Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
There is no searching out of the Ruler of all: his strength and his judging are great; he is full of righteousness, doing no wrong.
24 Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”
For this cause men go in fear of him; he has no respect for any who are wise in heart.