< Ayubu 36 >
1 Elihu aliendelea na kusema,
Y Añadió Eliú, y dijo:
2 “Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
Espérame un poco, y te enseñaré; porque todavía hablo por Dios.
3 Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
Tomaré mi sabiduría de lejos, y daré la justicia a mi hacedor.
4 Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
Porque de cierto no son mentira mis palabras; antes se trata contigo con perfecta sabiduría.
5 Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
He aquí que Dios es grande, y no aborrece; fuerte es en virtud de corazón.
6 Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
No dará vida al impío, antes a los humildes dará su derecho.
7 Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
No quitará sus ojos del justo; antes bien con los reyes los pondrá en silla para siempre, y serán ensalzados.
8 Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
Y si estuvieren presos en grillos, y cautivos en las cuerdas de la bajeza,
9 kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
él les anunciará la obra de ellos, y que sus rebeliones prevalecieron.
10 Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
Y despierta el oído de ellos para castigo, y les dice que se conviertan de la iniquidad.
11 Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
Si oyeren, y le sirvieren, acabarán sus días en bien, y sus años en deleites.
12 Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
Mas si no oyeren, serán pasados a cuchillo, y perecerán sin sabiduría.
13 Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
Pero los hipócritas de corazón lo irritarán más, y no clamarán cuando él los atare.
14 Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
Fallecerá el alma de ellos en su juventud, y su vida entre los fornicarios.
15 Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
Al pobre librará de su pobreza, y en la aflicción despertará su oído.
16 Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
Asimismo te apartaría de la boca de la angustia a lugar espacioso, libre de todo apuro; y te asentará mesa llena de grosura.
17 Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
Mas tú has llenado el juicio del impío, contra la justicia y el juicio que lo sustentan todo.
18 Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
Por lo cual de temer es que no te quite con golpe, el cual no puedas apartar de ti con gran rescate.
19 Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
¿Por ventura estimará él tus riquezas, ni del oro, ni de todas las fuerzas de la potencia?
20 Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
No anheles la noche, en la cual él corta los pueblos de su lugar.
21 Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
Guárdate, no mires a la iniquidad; teniéndola por mejor que la pobreza.
22 Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
He aquí que Dios es excelso con su potencia; ¿qué enseñador semejante a él?
23 Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
¿Quién le ha prescrito su camino? ¿Y quién le dirá: Iniquidad has hecho?
24 Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
Acuérdate de engrandecer su obra, la cual contemplan los hombres.
25 Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
La cual vieron todos los hombres; y el hombre la ve de lejos.
26 Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
He aquí, Dios es grande, y nosotros no le conocemos; ni se puede rastrear el número de sus años.
27 Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
Porque él detiene las goteras de las aguas, cuando la lluvia se derrama de su vapor;
28 ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
cuando gotean de las nubes, gotean sobre los hombres en abundancia.
29 Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
¿Si entenderá también los extendimientos de las nubes, y los bramidos de su tienda?
30 Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
He aquí que sobre él sobre extiende su luz, y cubrió las raíces del mar.
31 Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
Con ellas castiga a los pueblos, y da comida a la multitud.
32 Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
Con las nubes encubre la luz, y les manda que vayan contra ella.
33 Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.
La una da nuevas de la otra; la una adquiere ira contra la que viene.