< Ayubu 36 >

1 Elihu aliendelea na kusema,
Also Helyu addide, and spak these thingis,
2 “Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
Suffre thou me a litil, and Y schal schewe to thee; for yit Y haue that, that Y schal speke for God.
3 Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
Y schal reherse my kunnyng fro the bigynnyng; and Y schal preue my worchere iust.
4 Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
For verili my wordis ben with out leesyng, and perfit kunnyng schal be preued to thee.
5 Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
God castith not awei myyti men, sithen he is myyti;
6 Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
but he saueth not wickid men, and he yyueth dom to pore men.
7 Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
He takith not awei hise iyen fro a iust man; and he settith kyngis in seete with out ende, and thei ben reisid there.
8 Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
And if thei ben in chaynes, and ben boundun with the roopis of pouert,
9 kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
he schal shewe to hem her werkis, and her grete trespassis; for thei weren violent, `ethir rauenours.
10 Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
Also he schal opene her eere, that he chastise; and he schal speke, that thei turne ayen fro wickidnesse.
11 Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
If thei heren, and kepen, thei schulen fille her daies in good, and her yeris in glorie.
12 Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
Sotheli if thei heren not, thei schulen passe bi swerd, and thei schulen be wastid in foli.
13 Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
Feyneris and false men stiren the ire of God; and thei schulen not crye, whanne thei ben boundun.
14 Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
The soule of hem schal die in tempest; and the lijf of hem among `men of wymmens condiciouns.
15 Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
He schal delyuere a pore man fro his angwisch; and he schal opene `the eere of hym in tribulacioun.
16 Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
Therfor he schal saue thee fro the streit mouth of the broddeste tribulacioun, and not hauynge a foundement vndur it; sotheli the rest of thi table schal be ful of fatnesse.
17 Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
Thi cause is demed as the cause of a wickid man; forsothe thou schalt resseyue thi cause and doom.
18 Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
Therfor ire ouercome thee not, that thou oppresse ony man; and the multitude of yiftis bowe thee not.
19 Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
Putte doun thi greetnesse with out tribulacioun, and putte doun alle stronge men bi strengthe.
20 Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
Dilaie thou not nyyt, that puplis stie for hem.
21 Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
Be thou war, that thou bowe not to wickidnesse; for thou hast bigunne to sue this wickidnesse aftir wretchidnesse.
22 Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Lo! God is hiy in his strengthe, and noon is lijk hym among the yyueris of lawe.
23 Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
Who mai seke out the weies of God? ethir who dar seie to hym, Thou hast wrouyt wickidnesse?
24 Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
Haue thou mynde, that thou knowist not his werk, of whom men sungun.
25 Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
Alle men seen God; ech man biholdith afer.
26 Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
Lo! God is greet, ouercomynge oure kunnyng; the noumbre of hise yeeris is with out noumbre.
27 Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
Which takith awei the dropis of reyn; and schedith out reynes at the licnesse of floodyatis,
28 ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
whiche comen doun of the cloudis, that hilen alle thingis aboue.
29 Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
If he wole stretche forthe cloudis as his tente,
30 Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
and leite with his liyt fro aboue, he schal hile, yhe,
31 Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
the herris of the see. For bi these thingis he demeth puplis, and yyueth mete to many deedli men.
32 Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
In hondis he hidith liyt; and comaundith it, that it come eft.
33 Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.
He tellith of it to his freend, that it is his possessioun; and that he may stie to it.

< Ayubu 36 >