< Ayubu 36 >

1 Elihu aliendelea na kusema,
Elihu also proceeded, and said,
2 “Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
Bear with me a little, and I will show thee that I have yet to speak on God’s behalf.
3 Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
I will bring my knowledge from afar, and will ascribe righteousness to my Maker.
4 Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
For truly my words shall not be false: he that is perfect in knowledge is with thee.
5 Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
Behold, God is mighty, and despiseth not any: he is mighty in strength and wisdom.
6 Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
He preserveth not the life of the wicked: but giveth right to the poor.
7 Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
He withdraweth not his eyes from the righteous: but with kings are they on the throne; yea, he doth establish them for ever, and they are exalted.
8 Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
And if they are bound in fetters, and are held in cords of affliction;
9 kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
Then he showeth them their work, and their transgressions that they have exceeded.
10 Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
He openeth also their ear to discipline, and commandeth that they return from iniquity.
11 Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
If they obey and serve him, they shall spend their days in prosperity, and their years in pleasures.
12 Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
But if they obey not, they shall perish by the sword, and they shall die without knowledge.
13 Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
But the hypocrites in heart heap up wrath: they cry not when he bindeth them.
14 Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
They die in youth, and their life is among the sodomites.
15 Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
He delivereth the poor in his affliction, and openeth their ears in oppression.
16 Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
Even so would he have removed thee out of distress into a broad place, where there is no restraint; and that which should be set on thy table should be full of fatness.
17 Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
But thou hast fulfilled the judgment of the wicked: judgment and justice take hold on thee.
18 Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
Because there is wrath, beware lest he take thee away with his stroke: then a great ransom cannot deliver thee.
19 Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
Will he esteem thy riches? no, not gold, nor all the forces of strength.
20 Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
Desire not the night, when people are cut off in their place.
21 Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
Take heed, regard not iniquity: for this hast thou chosen rather than affliction.
22 Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Behold, God exalteth by his power: who teacheth like him?
23 Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
Who hath directed him his way? or who can say, Thou hast wrought iniquity?
24 Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
Remember that thou magnify his work, which men behold.
25 Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
Every man may see it; man may behold it afar off.
26 Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
Behold, God is great, and we know him not, neither can the number of his years be searched out.
27 Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
For he maketh small the drops of water: they pour down rain according to the vapour of it:
28 ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
Which the clouds do drop and distil upon man abundantly.
29 Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
Also can any understand the spreadings of the clouds, or the noise of his tabernacle?
30 Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
Behold, he spreadeth his light upon it, and covereth the bottom of the sea.
31 Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
For by them he judgeth the people; he giveth food in abundance.
32 Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
With clouds he covereth the light; and commandeth it not to shine by the cloud that cometh between.
33 Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.
The noise of it showeth concerning it, the cattle also concerning the vapour.

< Ayubu 36 >