< Ayubu 36 >
1 Elihu aliendelea na kusema,
Elihu also proceeded, and said:
2 “Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
Bear with me a little while, that I may show thee! For I have yet words in behalf of God.
3 Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
I will bring my knowledge from afar, And assert the justice of my Maker.
4 Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
Truly my words shall not be false: A man of sound knowledge is before thee.
5 Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
Behold, God is great, but despiseth not any; Great is he in strength of understanding.
6 Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
He suffereth not the wicked to prosper, But rendereth justice to the oppressed.
7 Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
He withdraweth not his eyes from the righteous; But establisheth them for ever with kings on the throne, That they may be exalted.
8 Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
And if they be bound in fetters, And holden in the cords of affliction,
9 kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
Then showeth he them their deeds, And how they have set him at defiance by their transgressions;
10 Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
He also openeth their ears to admonition, And commandeth them to return from iniquity.
11 Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
If they obey and serve him, They spend their days in prosperity, And their years in pleasures.
12 Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
But if they obey not, they perish by the sword; They die in their own folly.
13 Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
The corrupt in heart treasure up wrath; They cry not to God, when he bindeth them.
14 Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
They die in their youth; They close their lives with the unclean.
15 Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
But he delivereth the poor in their distress; He openeth their ears in affliction.
16 Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
He will bring thee also from the jaws of distress To a broad place, where is no straitness; And the provision of thy table shall be full of fatness.
17 Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
But if thou art full of the judgment of the wicked, Judgment and justice shall take hold of thee.
18 Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
For if wrath be with him, beware lest he take thee away by his stroke, So that a great ransom shall not save thee!
19 Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
Will he esteem thy riches? No! neither thy gold, nor all the abundance of thy wealth.
20 Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
Long not thou for that night To which nations are taken away from their place.
21 Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
Take heed, turn not thine eyes to iniquity! For this hast thou chosen rather than affliction.
22 Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Behold, God is exalted in his power: Who is a teacher like him?
23 Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
Who hath prescribed to him his way? Or who can say to him, “Thou hast done wrong”?
24 Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
Forget not to magnify his work, Which men celebrate with songs.
25 Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
All mankind gaze upon it; Mortals behold it from afar.
26 Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
Behold, God is great; we cannot know him, Nor search out the number of his years.
27 Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
Lo! he draweth up the drops of water, Which distil rain from his vapor;
28 ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
The clouds pour it down, And drop it upon man in abundance.
29 Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
Who can understand the spreading of his clouds, And the rattling of his pavilion?
30 Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
Behold, he spreadeth around himself his light, And he clotheth himself with the depths of the sea.
31 Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
By these he punisheth nations, And by these he giveth food in abundance.
32 Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
His hands he covereth with lightning; He giveth it commandment against an enemy.
33 Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.
His thunder maketh him known; Yea, to the herds, as he ascendeth on high.