< Ayubu 36 >

1 Elihu aliendelea na kusema,
And Elihu adds and says:
2 “Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
“Honor me a little, and I show you, That yet for God [are] words.
3 Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
I lift up my knowledge from afar, And I ascribe righteousness to my Maker.
4 Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
For my words [are] truly not false, The perfect in knowledge [is] with you.
5 Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
Behold, God [is] mighty, and does not despise, Mighty [in] power [and] heart.
6 Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
He does not revive the wicked, And appoints the judgment of the poor;
7 Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
He does not withdraw His eyes from the righteous, And [from] kings on the throne, And causes them to sit forever, and they are high,
8 Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
And if prisoners in chains They are captured with cords of affliction,
9 kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
Then He declares to them their work, And their transgressions, Because they have become mighty,
10 Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
And He uncovers their ear for instruction, And commands that they turn back from iniquity.
11 Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
If they hear and serve, They complete their days in good, And their years in pleasantness.
12 Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
And if they do not listen, They pass away by the dart, And expire without knowledge.
13 Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
And the profane in heart set the face, They do not cry when He has bound them.
14 Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
Their soul dies in youth, And their life among the defiled.
15 Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
He draws out the afflicted in his affliction, And uncovers their ear in oppression.
16 Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
And He also moved you from a narrow place [To] a broad place—no constriction under it, And the sitting beyond of your table has been full of fatness.
17 Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
And you have fulfilled the judgment of the wicked, Judgment and justice are upheld because of fury,
18 Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
Lest He move you with a stroke, And the abundance of an atonement not turn you aside.
19 Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
Does He value your riches? He has gold, and all the forces of power.
20 Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
Do not desire the night, For the going up of peoples in their stead.
21 Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
Take heed—do not turn to iniquity, For you have fixed on this Rather than [on] affliction.
22 Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Behold, God sits on high by His power, Who [is] like Him—a teacher?
23 Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
Who has appointed to Him His way? And who said, You have done iniquity?
24 Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
Remember that you magnify His work That men have beheld.
25 Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
All men have looked on it, Man looks attentively from afar.
26 Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
Behold, God [is] high, And we do not know the number of His years, Indeed, there [is] no searching.
27 Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
When He diminishes droppings of the waters, They refine rain according to its vapor,
28 ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
Which clouds drop, They distill on man abundantly.
29 Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
Indeed, do [any] understand The spreadings out of a cloud? The noises of His dwelling place?
30 Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
Behold, He has spread His light over it, And He has covered the roots of the sea,
31 Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
For He judges peoples by them, He gives food in abundance.
32 Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
By two palms He has covered the light, And lays a charge over it in meeting,
33 Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.
His shout shows it, The livestock also, the rising [storm].”

< Ayubu 36 >