< Ayubu 36 >
1 Elihu aliendelea na kusema,
Elihu continued speaking.
2 “Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
“Be patient with me just a little while longer and let me explain. I still have something to say on God's behalf.
3 Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
I will share my extensive knowledge, and I will prove my Creator is in the right.
4 Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
I assure you that what I'm saying are not lies, for I am a man whose knowledge is of the highest order.
5 Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
God is mighty, but doesn't despise anyone; he is powerful in strength and understanding.
6 Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
He does not keep the wicked alive, but gives justice to the oppressed.
7 Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
He always pays attention those who do right, and places them on thrones with kings, honoring them eternally.
8 Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
If they are bound in chains, tied down by ropes of suffering,
9 kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
then he explains to them what they've done—their arrogant sins.
10 Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
He makes them pay attention and orders them to stop sinning.
11 Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
If they listen and do what God says they will live out their lives in happiness.
12 Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
But if they do not listen they will die a violent death, ignorant of God.
13 Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
Those who reject God hold on to their bitterness. Even when he disciplines them they do not cry out to him for help.
14 Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
They die in their youth; their lives end among the male temple prostitutes.
15 Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
Through suffering God saves those who suffer; he gets their attention through their troubles.
16 Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
God is trying to rescue you from the jaws of trouble to a place of freedom and safety, filling your table full of the very best food.
17 Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
But you are preoccupied with the fate of the wicked; judgment and justice fill your mind.
18 Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
But be careful that your anger doesn't seduce you into mockery; and don't let the size of the ‘bribe’ lead you into sin.
19 Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
Will your cry for help sustain you when troubles come?
20 Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
Do not long for the night when people are suddenly taken away.
21 Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
Watch out that you don't turn to evil! For it's because of this that you are being tested through suffering.
22 Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Look how much power God has! What teacher is like him?
23 Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
Who has instructed him what to do? Who can say to him ‘You have done wrong’?
24 Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
Instead you should praise him for what he has done, as people have done in song.
25 Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
Everyone has seen God's creation, though only from a distance.
26 Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
See how great God is—more than we can understand! No one can count his years.
27 Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
He draws up the water and distils it into the dew and the rain.
28 ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
The clouds pour down rain, falling plentifully on humankind.
29 Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
Can anyone understand how the clouds spread out, or how thunder roars from where he lives?
30 Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
See how he scatters lightning around him, and covers the depths of the sea in darkness.
31 Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
By these actions he rules the people, he provides abundant food.
32 Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
He holds lightning in his hands and commands where it should strike.
33 Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.
Thunder declares his presence—even cattle know when a storm is coming.