< Ayubu 36 >
1 Elihu aliendelea na kusema,
Continuing in a similar manner, Eliu had this to say:
2 “Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
Bear with me for a little while and I will show you; for I have still more to say in favor of God.
3 Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
I will review my knowledge from the beginning, and I will prove my Maker to be just.
4 Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
For truly my words are without any falsehood and perfect knowledge will be proven to you.
5 Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
God does not abandon the powerful, for he himself is also powerful.
6 Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
But he does not save the impious, though he grants judgment to the poor.
7 Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
He will not take his eyes away from the just, and he continually establishes kings on their throne, and they are exalted.
8 Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
And, if they are in captivity, or are bound with the chains of poverty,
9 kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
he will reveal to them their works, as well as their sinfulness, in that they were violent.
10 Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
Likewise, he will open their ears to his correction, and he will speak to them, so that they may return from iniquity.
11 Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
If they listen and obey, they will fill their days with goodness and complete their years in glory.
12 Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
But if they will not listen, they will pass away by the sword and will be consumed by foolishness.
13 Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
The false and the crafty provoke the wrath of God, yet they do not cry out to him when they are chained.
14 Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
Their soul will die in a storm, and their life, among the unmanly.
15 Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
He will rescue the poor from his anguish, and he will open his ear during tribulation.
16 Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
Therefore, he will save you from the narrow mouth very widely, even though it has no foundation under it. Moreover, your respite at table will be full of fatness.
17 Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
Your case has been judged like that of the impious; you will withdraw your plea and your judgment.
18 Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
Therefore, do not let anger overwhelm you so that you oppress another; neither should you allow a multitude of gifts to influence you.
19 Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
Lay down your greatness without distress, and put aside all of your power with courage.
20 Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
Do not prolong the night, even if people rise on their behalf.
21 Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
Be careful that you do not turn to iniquity; for, after your misery, you have begun to follow this.
22 Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Behold, God is exalted in his strength, and there is no one like him among the law-givers.
23 Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
Who is able to investigate his ways? And who can say, “You have done iniquity,” to him?
24 Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
Remember that you are ignorant of his work, yet men have sung its praises.
25 Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
All men consider him; and each one ponders from a distance.
26 Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
Behold, God is great, defeating our knowledge; the number of his years is inestimable.
27 Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
He carries away the drops of rain, and he sends forth showers like a raging whirlpool;
28 ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
they flow from the clouds that are woven above everything.
29 Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
If he wills it, he extends the clouds as his tent
30 Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
and shines with his light from above; likewise, he covers the oceans within his tent.
31 Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
For he judges the people by these things, and he gives food to a multitude of mortals.
32 Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
Within his hands, he hides the light, and he commands it to come forth again.
33 Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.
He announces it to his friend, for it is his possession and he is able to reach out to it.