< Ayubu 35 >

1 Aidha, Elihu aliendelea kusema,
Entonces Elihú continuó diciendo:
2 “Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
“¿Crees que es honesto afirmar que tienes razón ante Dios?
3 Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
Y preguntas: ‘¿Qué beneficio obtengo? ¿De qué me ha servido no pecar?’
4 Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
“¡Te lo diré, y a tus amigos también!
5 Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
Sólo tienes que mirar al cielo y ver. Observa las nubes en lo alto.
6 Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
Si pecas, ¿en qué perjudica eso a Dios? ¿Cómo afectan tus muchos pecados a Dios?
7 Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
Si haces lo correcto, ¿qué bien le haces a él?
8 Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
No. Tus pecados sólo afectan a la gente como tú, y cualquier bien que hagas también les afecta a ellos.
9 Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
“La gente clama a causa de las terribles persecuciones, pide que alguien la salve de sus opresores.
10 Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
Pero nadie pregunta: ‘¿Dónde está mi Dios creador, el que inspira cantos en la noche,
11 ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
que nos enseña más que los animales y nos hace más sabios que las aves?’
12 Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
Cuando claman por ayuda, Dios no responde porque son gente orgullosa y malvada.
13 Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
Dios no escucha sus gritos vacíos; el Todopoderoso no les hace caso.
14 Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
¿Cuánto menos te escuchará Dios cuando le digas que no te ve? Tu caso está ante él, así que tienes que esperarlo.
15 Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
“Estás diciendo que Dios no castiga a la gente en su ira y presta poca atención al pecado.
16 Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”
Tú, Job, hablas sin sentido, haciendo largos discursos cuando no sabes nada!”

< Ayubu 35 >