< Ayubu 35 >
1 Aidha, Elihu aliendelea kusema,
Und wieder hob Elihu an und sprach:
2 “Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
"Ja, hältst du das für Recht und meinst du das mit 'meinem Rechthaben vor Gott'?
3 Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
Du sagst: 'Was nützt es Dir? Was nützt es mir, wenn ich nicht sündige?'
4 Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
Ich will dir drauf die Antwort geben und deinen Freunden hier bei dir.
5 Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
Schau auf zum Himmel; sieh! Blick zu den hohen Wolken über dir empor!
6 Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
Du hast gesündigt. Was tust du ihm damit? Sind deiner Sünden noch so viel, was machst du ihm damit?
7 Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
Und bist du fromm, was schenkst du ihm? Was nur empfängt er da aus deiner Hand?
8 Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
Doch deinesgleichen geht dein Frevel an, die Menschenkinder deine Frömmigkeit.
9 Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
Man schreit wohl über der Bedrückung Menge, führt Klage ob der Großen Macht.
10 Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
Doch niemand fragt: 'Wo bleibt da Gott, mein Schöpfer, der in der Nachtzeit spricht,
11 ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
der vor des Feldes Tieren uns belehrt, uns vor des Himmels Vögeln Weisheit schenkt?'
12 Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
Dann schreit man ob des Übermuts der Bösen; doch er schenkt kein Gehör.
13 Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
Zu nichts führt es, so sagst du, nimmer höre Gott, und der Allmächtige seh' dies Treiben nicht,
14 Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
zumal du sagst, du könnest ihn nicht sehen; der Streitfall liege ihm zwar vor, du aber müßtest immer auf ihn warten,
15 Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
und weil er sich nicht zeige, so strafe er im Zorne; er wolle nichts von Urteil wissen.
16 Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”
Da redet Job denn doch gar unvernünftig; er macht viel Redens ohne Einsicht."