< Ayubu 35 >
1 Aidha, Elihu aliendelea kusema,
Et Elihou, continuant dit:
2 “Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
Qu'as-tu pensé obtenir d'un jugement? Qui es-tu, toi qui as osé dire: Je suis juste devant le Seigneur?
3 Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
Quand tu dis: En quoi pécherai-je?
4 Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
Vous allez entendre la réponse, toi et tes trois amis.
5 Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
Lève les yeux au ciel et regarde; les nuées t'enseigneront combien les choses d'en haut sont loin de toi.
6 Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
Si tu pèches, quel danger court le Seigneur? Si tes fautes sont nombreuses, que pourras-tu faire contre lui?
7 Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
Si tu es juste, qu'en revient-il à Dieu? Que prendra-t-il de ta main?
8 Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
C'est l'homme, ton semblable, que ton impiété touche; c'est le fils de l'homme qu'intéresse ta justice.
9 Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
Les gens de mauvaise foi se plaindront de tout; ils crieront à l'oppression, à la violence.
10 Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
Et nul d'entre eux n'a dit: Où est Dieu, mon créateur, qui a mis en ordre les astres de la nuit,
11 ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
Qui m'a distingué des bêtes de la terre et des oiseaux du ciel?
12 Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
Ils crieront et il n'entendra pas; et ils se plaindront des outrages des méchants.
13 Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
Mais le Seigneur, le seul Tout-Puissant refuse de jeter un regard sur les choses vaines.
14 Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
Il voit tous ceux qui commettent des iniquités, et il me sauvera; soumets-toi à sa justice; puisses-tu le louer tel qu'il est maintenant pour toi.
15 Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
Car nul n'a le droit d'examiner sa colère ni de présumer qu'il fait quelque faux pas.
16 Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”
Job a donc témérairement ouvert la bouche, et son courroux provient de son ignorance des choses.