< Ayubu 35 >

1 Aidha, Elihu aliendelea kusema,
Moreover Elihu answered and said,
2 “Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
Thinkest thou this to be [thy] right, [or] sayest thou, My righteousness is more than God’s,
3 Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
That thou sayest, What advantage will it be unto thee? [and], What profit shall I have, more than if I had sinned?
4 Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
I will answer thee, and thy companions with thee.
5 Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
Look unto the heavens, and see; and behold the skies, which are higher than thou.
6 Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
If thou hast sinned, what doest thou against him? and if thy transgressions be multiplied, what doest thou unto him.
7 Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
If thou be righteous, what givest thou him? or what receiveth he of thine hand?
8 Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
Thy wickedness [may hurt] a man as thou art; and thy righteousness [may profit] a son of man.
9 Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
By reason of the multitude of oppressions they cry out; they cry for help by reason of the arm of the mighty.
10 Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
But none saith, Where is God my Maker, who giveth songs in the night;
11 ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
Who teacheth us more than the beasts of the earth, and maketh us wiser than the fowls of heaven?
12 Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
There they cry, but none giveth answer, because of the pride of evil men.
13 Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
Surely God will not hear vanity, neither will the Almighty regard it.
14 Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
How much less when thou sayest thou beholdest him not, the cause is before him, and thou waitest for him!
15 Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
But now, because he hath not visited in his anger, neither doth he greatly regard arrogance;
16 Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”
Therefore doth Job open his mouth in vanity; he multiplieth words without knowledge.

< Ayubu 35 >