< Ayubu 35 >

1 Aidha, Elihu aliendelea kusema,
And Elihu answers and says:
2 “Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
“Have you reckoned this for judgment [when] you have said, My righteousness [is] more than God’s?
3 Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
For you say, What does it profit You? What do I profit from my sin?
4 Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
I return words, and your friends with you,
5 Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
Behold attentively the heavens—and see, And behold the clouds, They have been higher than you.
6 Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
If you have sinned, what do you do against Him? And your transgressions have been multiplied, What do you do to Him?
7 Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
If you have been righteous, What do you give to Him? Or what does He receive from your hand?
8 Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
For a man like yourself [is] your wickedness, And for a son of man your righteousness.
9 Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
Because of the multitude of oppressions They cause to cry out, They cry because of the arm of the mighty.
10 Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
And none said, Where [is] God my Maker? Giving songs in the night,
11 ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
Teaching us more than the beasts of the earth, Indeed, He makes us wiser than the bird of the heavens.
12 Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
There they cry, and He does not answer, Because of the pride of evildoers.
13 Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
Surely God does not hear vanity, And the Mighty does not behold it.
14 Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
Indeed, though you say you do not behold Him, Judgment [is] before Him, and stays for Him.
15 Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
And now, because there is not, He has appointed His anger, And He has not known in great extremity.
16 Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”
And Job opens his mouth [with] vanity, He multiplies words without knowledge.”

< Ayubu 35 >