< Ayubu 34 >

1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
Још говори Елијуј и рече:
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Чујте, мудри, беседу моју, и разумни послушајте ме.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
Јер ухо познаје беседу као што грло куша јело.
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Разаберимо шта је право, извидимо међу собом шта је добро.
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
Јер Јов рече: Праведан сам, а Бог одбаци моју правду.
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
Хоћу ли лагати за своју правду? Стрела је моја смртна, а без кривице.
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
Који је човек као Јов да као воду пије подсмех?
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
И да се дружи с онима који чине безакоње, и да ходи с безбожним људима?
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
Јер рече: Не помаже човеку да угађа Богу.
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Зато, људи разумни, послушајте ме; далеко је од Бога злоћа и неправда од Свемогућег.
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
Јер по делу плаћа човеку и даје сваком да нађе према путу свом.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
Доиста Бог не ради зло и Свемогући не изврће правде.
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
Ко Му је предао земљу? И ко је уредио васиљену?
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
Кад би на себе окренуо срце своје, узео би к себи дух свој и дисање своје;
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
Изгинуло би свако тело, и човек би се вратио у прах.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
Ако си, дакле, разуман, чуј ово: слушај глас речи мојих.
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
Може ли владати онај који мрзи на правду? Хоћеш ли осудити оног који је најправеднији?
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
Каже ли се цару: Ниткове! И кнезовима: Безбожници?
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
А камо ли Ономе који не гледа кнезовима ко су, нити у Њега вреди више богати од сиромаха, јер су сви дело руку Његових.
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
Умиру за час, и у по ноћи усколеба се народ и пропадне, и однесе се јаки без руке људске.
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
Јер су очи Његове обраћене на путеве човечије и види све кораке његове.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
Нема мрака ни сена смртнога где би се сакрили који чине безакоње.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
Јер никоме не одгађа кад дође да се суди с Богом.
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
Сатире јаке недокучиво, и поставља друге на њихово место.
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
Јер зна дела њихова, и док обрати ноћ, сатру се.
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
Као безбожне разбија их на видику.
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
Јер одступише од Њега и не гледаше ни на које путеве Његове;
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
Те дође до Њега вика сиромахова, и чу вику невољних.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
Кад Он умири, ко ће узнемирити? И кад Он сакрије лице, ко ће Га видети? И то бива и народу и човеку.
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
Да не би царовао лицемер, да не би било замке народу.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
Заиста, треба казати Богу: Подносио сам, нећу више грешити.
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
А шта не видим, Ти ме научи; ако сам чинио неправду, нећу више.
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
Еда ли ће по теби плаћати, јер теби није по вољи, јер ти бираш а не Он? Ако знаш шта, говори.
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Људи ће разумни са мном казати, и мудар ће човек пристати,
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
Да Јов не говори разумно, и да речи његове нису мудре.
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
Оче мој, нека се Јов искуша до краја, што одговара као зли људи.
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
Јер домеће на грех свој безакоње, пљеска рукама међу нама, и много говори на Бога.

< Ayubu 34 >