< Ayubu 34 >

1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
Eliu continuò a dire:
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Ascoltate, saggi, le mie parole e voi, sapienti, porgetemi l'orecchio,
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
Perché l'orecchio distingue le parole, come il palato assapora i cibi.
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Esploriamo noi ciò che è giusto, indaghiamo fra di noi quale sia il bene:
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
poiché Giobbe ha detto: «Io son giusto, ma Dio mi ha tolto il mio diritto;
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
contro il mio diritto passo per menzognero, inguaribile è la mia piaga benché senza colpa».
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
Chi è come Giobbe che beve, come l'acqua, l'insulto,
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
che fa la strada in compagnia dei malfattori, andando con uomini iniqui?
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
Poiché egli ha detto: «Non giova all'uomo essere in buona grazia con Dio».
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Perciò ascoltatemi, uomini di senno: lungi da Dio l'iniquità e dall'Onnipotente l'ingiustizia!
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
Poiché egli ripaga l'uomo secondo il suo operato e fa trovare ad ognuno secondo la sua condotta.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
In verità, Dio non agisce da ingiusto e l'Onnipotente non sovverte il diritto!
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
Chi mai gli ha affidato la terra e chi ha disposto il mondo intero?
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
Se egli richiamasse il suo spirito a sè e a sé ritraesse il suo soffio,
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
ogni carne morirebbe all'istante e l'uomo ritornerebbe in polvere.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
Se hai intelletto, ascolta bene questo, porgi l'orecchio al suono delle mie parole.
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
Può mai governare chi odia il diritto? E tu osi condannare il Gran Giusto?
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
lui che dice ad un re: «Iniquo!» e ai principi: «Malvagi!»,
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
lui che non usa parzialità con i potenti e non preferisce al povero il ricco, perché tutti costoro sono opera delle sue mani?
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
In un istante muoiono e nel cuore della notte sono colpiti i potenti e periscono; e senza sforzo rimuove i tiranni,
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
poiché egli tiene gli occhi sulla condotta dell'uomo e vede tutti i suoi passi.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
Non vi è tenebra, non densa oscurità, dove possano nascondersi i malfattori.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
Poiché non si pone all'uomo un termine per comparire davanti a Dio in giudizio:
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
egli fiacca i potenti, senza fare inchieste, e colloca altri al loro posto.
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
Poiché conosce le loro opere, li travolge nella notte e sono schiacciati;
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
come malvagi li percuote, li colpisce alla vista di tutti;
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
perché si sono allontanati da lui e di tutte le sue vie non si sono curati,
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
sì da far giungere fino a lui il grido dell'oppresso e fargli udire il lamento dei poveri.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
Se egli tace, chi lo può condannare? Se vela la faccia, chi lo può vedere? Ma sulle nazioni e sugli individui egli veglia,
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
perché non regni un uomo perverso, perché il popolo non abbia inciampi.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
Si può dunque dire a Dio: «Porto la pena, senza aver fatto il male;
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
se ho peccato, mostramelo; se ho commesso l'iniquità, non lo farò più»?
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
Forse, secondo le tue idee dovrebbe ricompensare, perché tu rifiuti il suo giudizio? Poiché tu devi scegliere, non io, dì, dunque, quello che sai.
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Gli uomini di senno mi diranno con l'uomo saggio che mi ascolta:
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
«Giobbe non parla con sapienza e le sue parole sono prive di senno».
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
Bene, Giobbe sia esaminato fino in fondo, per le sue risposte da uomo empio,
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
perché aggiunge al suo peccato la rivolta, in mezzo a noi batte le mani e moltiplica le parole contro Dio.

< Ayubu 34 >