< Ayubu 34 >
1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
Und Elihu hob wieder an und sprach:
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Höret, ihr Weisen, meine Worte, und ihr Kundigen, gebet mir Gehör!
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
Denn das Ohr prüft die Worte, wie der Gaumen die Speise kostet. [Eig. speisend kostet]
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Erwählen wir für uns, was recht, erkennen wir unter uns, was gut ist!
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
Denn Hiob hat gesagt: Ich bin gerecht, und Gott [El] hat mir mein Recht entzogen.
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
Trotz meines Rechtes soll ich lügen; meine Wunde [Eig. mein Pfeil; vergl. Kap. 6,4;16,13] ist unheilbar, ohne daß ich übertreten habe. -
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
Wer ist ein Mann wie Hiob, der Hohn trinkt wie Wasser,
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
und in Gesellschaft geht mit denen, die Frevel tun, und wandelt mit gottlosen Menschen?
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
Denn er hat gesagt: Keinen Nutzen hat ein Mann davon, daß er Wohlgefallen an Gott hat! [Eig. gern mit Gott verkehrt]
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Darum höret mir zu, ihr Männer von Verstand! Fern sei Gott von Gesetzlosigkeit, und der Allmächtige von Unrecht!
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
Sondern des Menschen Tun vergilt er ihm, und nach jemandes Wege läßt er es ihn finden.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
Ja, wahrlich, Gott [El] handelt nicht gesetzlos, und der Allmächtige beugt nicht das Recht.
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
Wer hat ihm die Erde anvertraut? Und wer den ganzen Erdkreis gegründet? [Eig. gesetzt]
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
Wenn er sein Herz nur auf sich selbst richtete, seinen Geist [O. Hauch] und seinen Odem an sich zurückzöge,
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
so würde alles Fleisch insgesamt verscheiden, und der Mensch zum Staube zurückkehren.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
Und wenn du doch dieses einsehen und hören, der Stimme meiner Worte Gehör schenken wolltest!
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
Sollte auch herrschen, wer das Recht haßt? oder willst du den Allgerechten [W. den Gerecht-Mächtigen] verdammen?
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
Sagt man zu einem Könige: Belial, [Nichtswürdiger] zu Edlen: Du Gottloser? -
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
Wieviel weniger zu ihm, der die Person der Fürsten nicht ansieht und den Reichen [O. Vornehmen] nicht vor dem Armen berücksichtigt! Denn sie alle sind das Werk seiner Hände.
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
In einem Augenblick sterben sie; und in der Mitte der Nacht wird ein Volk erschüttert und vergeht, und Mächtige werden beseitigt ohne Hand. [Eig. nicht durch Hand [d. h. Menschenhand]]
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
Denn seine Augen sind auf die Wege des Menschen gerichtet, und er sieht alle seine Schritte.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
Da ist keine Finsternis und kein Todesschatten, daß sich darein verbergen könnten, die Frevel tun.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
Denn er braucht nicht lange auf einen Menschen acht zu geben, damit er vor Gott [El] ins Gericht komme.
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
Er zerschmettert Gewaltige ohne Untersuchung, und setzt andere an ihre Stelle.
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
Daher kennt er ihre Handlungen, und kehrt sie um über Nacht; und sie werden zermalmt.
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
Er schlägt sie, wie Übeltäter, auf öffentlichem Platze,
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
darum daß sie von seiner Nachfolge [Eig. von hinter ihm] abgewichen sind [And. üb.: denn darum sind sie usw.] und alle seine Wege nicht bedacht haben,
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
um zu ihm hinaufdringen zu lassen das Schreien des Armen, und damit er das Schreien der Elenden höre.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
Schafft er Ruhe, wer will beunruhigen? Und verbirgt er das Angesicht, wer kann ihn schauen? So handelt er sowohl gegen ein Volk, als auch gegen einen Menschen zumal,
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
damit der ruchlose Mensch nicht regiere, damit sie nicht Fallstricke des Volkes seien.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
Denn hat er wohl zu Gott [El] gesagt: Ich trage meine Strafe, ich will nicht mehr verderbt handeln;
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
was ich nicht sehe, zeige du mir; wenn ich Unrecht verübt habe, so will ich es nicht mehr tun? -
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
Soll nach deinem Sinne er es vergelten? Denn du hast seine Vergeltung verworfen, und so mußt du wählen, [W. denn du hast verworfen, denn du mußt wählen] und nicht ich; was du weißt, reden denn!
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Männer von Verstand werden zu mir sagen, und ein weiser Mann, der mir zuhört:
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
Hiob redet nicht mit Erkenntnis, und seine Worte sind ohne Einsicht.
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
Ach, daß doch Hiob fort und fort geprüft würde wegen seiner Antworten nach Frevlerart!
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
Denn er fügt seiner Sünde Übertretung [O. Vermessenheit] hinzu, klatscht unter uns in die Hände und mehrt seine Worte gegen Gott. [El]