< Ayubu 34 >

1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
Élihu reprit et dit:
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Sages, écoutez mes discours! Vous qui êtes intelligents, prêtez-moi l’oreille!
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
Car l’oreille discerne les paroles, Comme le palais savoure les aliments.
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Choisissons ce qui est juste, Voyons entre nous ce qui est bon.
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
Job dit: Je suis innocent, Et Dieu me refuse justice;
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
J’ai raison, et je passe pour menteur; Ma plaie est douloureuse, et je suis sans péché.
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
Y a-t-il un homme semblable à Job, Buvant la raillerie comme l’eau,
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
Marchant en société de ceux qui font le mal, Cheminant de pair avec les impies?
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
Car il a dit: Il est inutile à l’homme De mettre son plaisir en Dieu.
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Écoutez-moi donc, hommes de sens! Loin de Dieu l’injustice, Loin du Tout-Puissant l’iniquité!
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
Il rend à l’homme selon ses œuvres, Il rétribue chacun selon ses voies.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
Non certes, Dieu ne commet pas l’iniquité; Le Tout-Puissant ne viole pas la justice.
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
Qui l’a chargé de gouverner la terre? Qui a confié l’univers à ses soins?
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
S’il ne pensait qu’à lui-même, S’il retirait à lui son esprit et son souffle,
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
Toute chair périrait soudain, Et l’homme rentrerait dans la poussière.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
Si tu as de l’intelligence, écoute ceci, Prête l’oreille au son de mes paroles!
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
Un ennemi de la justice régnerait-il? Et condamneras-tu le juste, le puissant,
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
Qui proclame la méchanceté des rois Et l’iniquité des princes,
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
Qui n’a point égard à l’apparence des grands Et ne distingue pas le riche du pauvre, Parce que tous sont l’ouvrage de ses mains?
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
En un instant, ils perdent la vie; Au milieu de la nuit, un peuple chancelle et périt; Le puissant disparaît, sans la main d’aucun homme.
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
Car Dieu voit la conduite de tous, Il a les regards sur les pas de chacun.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
Il n’y a ni ténèbres ni ombre de la mort, Où puissent se cacher ceux qui commettent l’iniquité.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
Dieu n’a pas besoin d’observer longtemps, Pour qu’un homme entre en jugement avec lui;
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
Il brise les grands sans information, Et il met d’autres à leur place;
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
Car il connaît leurs œuvres. Il les renverse de nuit, et ils sont écrasés;
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
Il les frappe comme des impies, A la face de tous les regards.
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
En se détournant de lui, En abandonnant toutes ses voies,
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
Ils ont fait monter à Dieu le cri du pauvre, Ils l’ont rendu attentif aux cris des malheureux.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
S’il donne le repos, qui répandra le trouble? S’il cache sa face, qui pourra le voir? Il traite à l’égal soit une nation, soit un homme,
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
Afin que l’impie ne domine plus, Et qu’il ne soit plus un piège pour le peuple.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
Car a-t-il jamais dit à Dieu: J’ai été châtié, je ne pécherai plus;
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
Montre-moi ce que je ne vois pas; Si j’ai commis des injustices, je n’en commettrai plus?
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
Est-ce d’après toi que Dieu rendra la justice? C’est toi qui rejettes, qui choisis, mais non pas moi; Ce que tu sais, dis-le donc!
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Les hommes de sens seront de mon avis, Le sage qui m’écoute pensera comme moi.
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
Job parle sans intelligence, Et ses discours manquent de raison.
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
Qu’il continue donc à être éprouvé, Puisqu’il répond comme font les méchants!
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
Car il ajoute à ses fautes de nouveaux péchés; Il bat des mains au milieu de nous, Il multiplie ses paroles contre Dieu.

< Ayubu 34 >