< Ayubu 34 >

1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
And Elihu proceeded, and said:
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Hear my words, ye wise men! Give ear to me, ye that have knowledge!
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
For the ear trieth words, As the mouth tasteth meat.
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Let us examine for ourselves what is right; Let us know among ourselves what is true.
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
Job hath said, “I am righteous, And God refuseth me justice.
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
Though I am innocent, I am made a liar; My wound is incurable, though I am free from transgression.”
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
Where is the man like Job, Who drinketh impiety like water;
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
Who goeth in company with evil-doers, And walketh with wicked men?
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
For he hath said, “A man hath no advantage, When he delighteth himself in God.”
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Wherefore hearken to me, ye men of understanding! Far be iniquity from God; Yea, far be injustice from the Almighty!
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
For what a man hath done he will requite him, And render to every one according to his deeds.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
Surely God will not do iniquity, Nor will the Almighty pervert justice.
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
Who hath given him the charge of the earth? Or who hath created the whole world?
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
Should he set his heart against man, Should he take back his spirit and his breath,
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
Then would all flesh expire together; Yea, man would return to the dust.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
If thou hast understanding, hear this! Give ear to the voice of my words!
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
Shall he, that hateth justice, govern? Wilt thou then condemn the just and mighty One?
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
Is it fit to say to a king, Thou art wicked; Or to princes, Ye are unrighteous?
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
How much less to him that is not partial to princes, Nor regardeth the rich more than the poor? For they are all the work of his hands.
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
In a moment they die; yea, at midnight Do the people stagger and pass away, And the mighty are destroyed without hand.
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
For his eyes are upon the ways of man; He seeth all his steps.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
There is no darkness, nor shadow of death, Where evil-doers may hide themselves.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
He needeth not attend long to a man, That he may go into judgment before God;
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
He dasheth in pieces the mighty without inquiry, And setteth up others in their stead.
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
Therefore he knoweth their works, And in a night he overthroweth them, so that they are destroyed.
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
On account of their wickedness he smiteth them, In the presence of many beholders;
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
Because they turned away from him, And had no regard to his ways,
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
And caused the cry of the poor to come before him; For he heareth the cry of the oppressed.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
When he giveth rest, who can cause trouble? And when he hideth his face, Who can behold him?
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
So is it with nations and individuals alike! That the wicked may no more rule, And may not be snares to the people.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
Surely thou shouldst say unto God, “I have received chastisement; I will no more offend;
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
What I see not, teach thou me! If I have done iniquity, I will do it no more.”
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
Shall he recompense according to thy mind, Because thou refusest, or because thou choosest, and not he? Speak, if thou hast knowledge!
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Men of understanding, Wise men, who hear me, will say,
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
“Job hath spoken without knowledge, And his words are without wisdom.”
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
I desire that Job may be tried to the last, For answering like wicked men.
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
For he addeth impiety to his sin; He clappeth his hands among us, And multiplieth words against God.

< Ayubu 34 >