< Ayubu 34 >

1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
And Elius continued, and said,
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Hear me, you wise men; listen, you that have knowledge.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
For the ear tries words, and the mouth tastes meat.
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Let us choose judgment to ourselves: let us know amount ourselves what is right.
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
For Job has said, I am righteous: the Lord has removed my judgment.
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
And he has erred in my judgment: my wound is severe without unrighteousness [of mine].
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
What man is as Job, drinking scorning like water?
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
[saying], I have not sinned, nor committed ungodliness, nor had fellowship with workers of iniquity, to go with the ungodly.
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
For you should not say, There shall be no visitation of a man, whereas [there is] a visitation on him from the Lord.
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Therefore hear me, you that are wise in heart: far be it from me to sin before the Lord, and to pervert righteousness before the almighty.
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
Yes, he renders to a man accordingly as each of them does, and in a man's path he will find him.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
And think you that the Lord will do wrong, or will the Almighty who made the earth wrest judgment?
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
And who is he that made [the whole world] under heaven, and all things therein?
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
For if he would confine, and restrain his spirit with himself;
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
all flesh would die together, and every mortal would return to the earth, whence also he was formed.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
Take heed lest he rebuke [you]: hear this, listen to the voice of words.
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
Behold then the one that hates iniquities, and that destroys the wicked, who is for ever just.
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
[He is] ungodly that says to a king, You are a transgressor, [that says] to princes, O most ungodly one.
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
[Such a one] as would not reverence the face of an honorable man, neither knows how to give honor to the great, so as that their persons should be respected.
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
But it shall turn out vanity to them, to cry and beseech a man; for they dealt unlawfully, the poor being turned aside [from their right].
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
For he surveys the works of men, and nothing of what they do has escaped him.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
Neither shall there be a place for the workers of iniquity to hide themselves.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
For he will not lay upon a man more [than right].
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
For the Lord looks down upon all men, who comprehends unsearchable things, glorious also and excellent things without number.
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
Who discovers their works, and will bring night about [upon them], and they shall be brought low.
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
And he quite destroys the ungodly, for they are seen before him.
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
Because they turned aside from the law of God, and did not regard his ordinances,
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
so as to bring before him the cry of the needy; for he will hear the cry of the poor.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
And he will give quiet, and who will condemn? and he will hide his face, and who shall see him? whether [it be done] against a nation, or against a man also:
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
causing a hypocrite to be king, because of the waywardness of the people.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
For [there is] one that says to the Mighty One, I have received [blessings]; I will not take a pledge:
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
I will see apart from myself: do you show me if I have done unrighteousness; I will not do [so] any more.
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
Will he take vengeance for it on you, whereas you will put [it] far [from you]? for you shall choose, and not I; and what you know, speak you.
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Because the wise in heart shall say this, and a wise man listens to my word.
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
But Job has not spoken with understanding, his words are not [uttered] with knowledge.
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
Howbeit do you learn, Job: no longer make answer as the foolish:
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
that we add not to our sins: for iniquity will be reckoned against us, if [we] speak many words before the Lord.

< Ayubu 34 >