< Ayubu 34 >
1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
Fremdeles svarede Elihu og sagde:
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Hører, I vise! min Tale, og I forstandige! vender eders Øren til mig;
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
thi Øret prøver Talen, og Ganen smager Maden.
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Lader os vælge os det rette, lader os kende imellem os, hvad godt er.
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
Thi Job sagde: Jeg er retfærdig, men Gud har borttaget min Ret.
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
Uagtet jeg har Ret, skal jeg staa som en Løgner; ulægelig har Pilen truffet mig, skønt der ikke er Overtrædelse hos mig.
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
Hvor er en Mand som Job, der inddrikker Gudsbespottelse som Vand
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
og vandrer i Selskab med dem, som gøre Uret, og gaar med ugudelige Folk?
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
Thi han sagde: Det gavner ikke en Mand, om han har Behag i Gud.
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Derfor, I Mænd af Forstand! hører paa mig: Det være langt fra Gud at være ugudelig, og fra den Almægtige at være uretfærdig.
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
Thi han betaler et Menneske efter dets Gerning og lader enhver faa efter hans Vej.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
Ja, sandelig, Gud handler ikke uretfærdigt, og den Almægtige forvender ikke Retten.
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
Hvo har beskikket ham over Jorden? og hvo har grundet hele Jordens Kreds.
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
Dersom han vilde agte paa sig selv alene, samlede han sin Aand og sin Aande til sig:
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
Da maatte alt Kød til Hobe opgive Aanden, og Mennesket blive til Støv igen.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
Dersom du har Forstand, saa hør dette, vend dine Øren til min Tales Røst!
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
Skulde vel den, som hader Ret, holde Styr? eller tør du sige den mægtige retfærdige at være uretfærdig?
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
Tør nogen sige til en Konge: Du Belial! til de ædle: Du ugudelige!
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
Han anser ikke Fyrsternes Personer og agter ikke den rige fremfor den ringe; thi de ere alle hans Hænders Gerning.
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
De dø i et Øjeblik, og det midt om Natten: Folk rystes og forgaa; og de mægtige tages bort, men ikke ved Menneskehaand.
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
Thi hans Øjne ere over hver Mands Veje, og han ser alle hans Skridt.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
Der er intet Mørke og ingen Dødsskygge, hvori de som gøre Uret, kunne skjule sig.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
Thi han behøver ikke at agte længe nogen, der skal stedes til Dom for Gud.
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
Han sønderslaar de mægtige uden at ransage, og han sætter andre i deres Sted.
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
Derfor kender han deres Gerninger og omkaster dem om Natten, at de blive knuste;
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
han slaar dem, hvor de ugudelige findes, paa det Sted, hvor Folk ser det.
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
Thi derfor vege de fra ham og agtede ikke paa nogen af hans Veje,
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
for at de kunde bringe den ringes Skrig ind for ham, og for at han maatte høre de elendiges Skrig.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
Naar han skaffer Ro til Veje — hvo vil kalde ham uretfærdig? — og naar han skjuler sit Ansigt — hvo kan da beskue ham? — baade for et Folk og for et enkelt Menneske:
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
Saa er det, for at en vanhellig ikke skal regere, og at der ikke skal være Snarer for Folket.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
Mon nogen har sagt til Gud: Jeg har faaet, hvad jeg ikke forskylder?
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
Lær du mig ud over det, jeg kan se; dersom jeg har gjort Uret, da vil jeg ikke gøre det mere.
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
Skal det være efter dit Skøn, at han skal gengælde? thi du har vraget, saa at du har at vælge, og ikke jeg? saa tal da, hvad du ved!
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Folk af Forstand skulle sige til mig, og ligeledes den vise Mand, som hører mig:
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
„Job taler ikke med Forstand, og hans Ord ere ikke mere Klogskab”.
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
O gid, at Job maatte prøves til fulde, fordi han har svaret som uretfærdige Mænd!
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
thi han lægger Overtrædelse til sin Synd, imellem os klapper han i Hænderne og gør mange Ord imod Gud.