< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
POR tanto, Job, oye ahora mis razones, y escucha todas mis palabras.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
He aquí yo abriré ahora mi boca, y mi lengua hablará en mi garganta.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
Mis razones [declararán] la rectitud de mi corazón, y mis labios proferirán pura sabiduría.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
El espíritu de Dios me hizo, y la inspiración del Omnipotente me dió vida.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
Si pudieres, respóndeme; dispón [tus palabras], está delante de mí.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Heme aquí á mí en lugar de Dios, conforme á tu dicho: de lodo soy yo también formado.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
He aquí que mi terror no te espantará, ni mi mano se agravará sobre ti.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
De cierto tú dijiste á oídos míos, y yo oí la voz de tus palabras [que decían]:
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
Yo soy limpio y sin defecto; y soy inocente, y no hay maldad en mí.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
He aquí que él buscó achaques contra mí, y me tiene por su enemigo;
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
Puso mis pies en el cepo, y guardó todas mis sendas.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
He aquí en esto no has hablado justamente: yo te responderé que mayor es Dios que el hombre.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
¿Por qué tomaste pleito contra él? Porque él no da cuenta de ninguna de sus razones.
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
Sin embargo, en una ó en dos [maneras] habla Dios; [mas el hombre] no entiende.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
Por sueño de visión nocturna, cuando el sueño cae sobre los hombres, cuando se adormecen sobre el lecho;
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Entonces revela al oído de los hombres, y les señala su consejo;
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
Para quitar al hombre de [su] obra, y apartar del varón la soberbia.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
Detendrá su alma de corrupción, y su vida de que pase á cuchillo.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
También sobre su cama es castigado con dolor fuerte en todos sus huesos,
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
Que le hace que su vida aborrezca el pan, y su alma la comida suave.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
Su carne desfallece sin verse, y sus huesos, que antes no se veían, aparecen.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
Y su alma se acerca al sepulcro, y su vida á los que causan la muerte.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
Si tuviera cerca de él [algún] elocuente anunciador muy escogido, que anuncie al hombre su deber;
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
Que le diga que [Dios] tuvo de él misericordia, que lo libró de descender al sepulcro, que halló redención:
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Enterneceráse su carne más que de niño, volverá á los días de su mocedad.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
Orará á Dios, y le amará, y verá su faz con júbilo: y él restituirá al hombre su justicia.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
El mira sobre los hombres; y [el que] dijere: Pequé, y pervertí lo recto, y no me ha aprovechado;
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
[Dios] redimirá su alma, que no pase al sepulcro, y su vida se verá en luz.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
He aquí, todas estas cosas hace Dios dos y tres veces con el hombre;
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
Para apartar su alma del sepulcro, y para iluminarlo con la luz de los vivientes.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Escucha, Job, y óyeme; calla, y yo hablaré.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
Que si tuvieres razones, respóndeme: habla, porque yo te quiero justificar.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
Y si no, óyeme tú á mí; calla, y enseñarte he sabiduría.

< Ayubu 33 >