< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
“Sin embargo, Job, escucha mi discurso, y escucha todas mis palabras.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Mira ahora, he abierto mi boca. Mi lengua ha hablado en mi boca.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
Mis palabras expresarán la rectitud de mi corazón. Lo que mis labios saben que hablarán con sinceridad.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
El Espíritu de Dios me ha hecho, y el aliento del Todopoderoso me da la vida.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
Si puedes, respóndeme. Pon en orden tus palabras ante mí, y levántate.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
He aquí que yo soy para con Dios lo mismo que vosotros. Yo también estoy formado de la arcilla.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
He aquí que mi terror no te hará temer, ni mi presión será pesada para ti.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
“Ciertamente, has hablado a mi oído, He escuchado la voz de tus palabras, diciendo,
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
‘Estoy limpio, sin desobediencia. Soy inocente y no hay iniquidad en mí.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
He aquí que encuentra ocasiones contra mí. Me cuenta como su enemigo.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
Pone mis pies en el cepo. Él marca todos mis caminos”.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
“He aquí que yo te responderé. En esto no eres justo, porque Dios es más grande que el hombre.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
¿Por qué os esforzáis contra él? porque no da cuenta de ninguno de sus asuntos?
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
Porque Dios habla una vez, sí dos veces, aunque el hombre no presta atención.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
En un sueño, en una visión nocturna, cuando el sueño profundo cae sobre los hombres, en el sueño en la cama,
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
entonces abre los oídos de los hombres, y sella su instrucción,
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
para que retire al hombre de su propósito, y ocultar el orgullo del hombre.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
Aleja su alma de la fosa, y su vida de perecer por la espada.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
“También es castigado con dolor en su cama, con una lucha continua en sus huesos,
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
para que su vida aborrezca el pan, y su alma un alimento delicado.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
Su carne está tan consumida que no se puede ver. Sus huesos que no se vieron sobresalen.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
Sí, su alma se acerca a la fosa, y su vida a los destructores.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
“Si hay junto a él un ángel, un intérprete, uno entre mil, para mostrar al hombre lo que es correcto para él,
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
entonces Dios se apiada de él y le dice, Líbralo de bajar a la fosa, He encontrado un rescate”.
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Su carne será más fresca que la de un niño. Vuelve a los días de su juventud.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
Reza a Dios, y éste le es favorable, para que vea su rostro con alegría. Él devuelve al hombre su justicia.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
Canta ante los hombres y dice, He pecado y he pervertido lo que era justo, y no me benefició.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
Él ha redimido mi alma de ir a la fosa. Mi vida verá la luz”.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
“He aquí que Dios hace todas estas cosas, dos veces, sí tres veces, con un hombre,
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
para sacar su alma de la fosa, para que sea iluminado con la luz de los vivos.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Fíjate bien, Job, y escúchame. Guarda silencio, y yo hablaré.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
Si tienes algo que decir, respóndeme. Habla, pues deseo justificarte.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
Si no, escúchame. Guarda la paz, y yo te enseñaré la sabiduría”.

< Ayubu 33 >