< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
Portanto, Jó, ouve, por favor, meus dizeres, e dá ouvidos a todas as minhas palavras.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Eis que já abri minha boca; minha língua já fala debaixo do meu céu da boca.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
Meus dizeres pronunciarão a integridade do meu coração, e o puro conhecimento dos meus lábios.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
O Espírito de Deus me fez, e o sopro do Todo-Poderoso me deu vida.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
Se puderes, responde-me; dispõe-te perante mim, e persiste.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Eis que para Deus eu sou como tu; do barro também eu fui formado.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Eis que meu terror não te espantará, nem minha mão será pesada sobre ti.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
Certamente tu disseste a meus ouvidos, e eu ouvi a voz de tuas palavras,
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
[Que diziam]: Eu sou limpo e sem transgressão; sou inocente, e não tenho culpa.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Eis que [Deus] buscou pretextos contra mim, [e] me tem por seu inimigo.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
Ele pôs meus pés no tronco, e observa todas as minhas veredas.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
Eis que nisto não foste justo, eu te respondo; pois Deus é maior que o ser humano.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Por que razão brigas contra ele por não dar resposta às palavras do ser humano?
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
Contudo Deus fala uma ou duas vezes, ainda que [o ser humano] não entenda.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
Em sonho [ou em] visão noturna, quando o sono profundo cai sobre as pessoas, [e] adormecem na cama.
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Então o revela ao ouvido das pessoas, e os sela com advertências;
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
Para desviar ao ser humano de sua obra, e do homem a soberba.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
Para desviar a sua alma da perdição, e sua vida de passar pela espada.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
Também em sua cama é castigado com dores, com luta constante em seus ossos,
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
De modo que sua vida detesta [até] o pão, e sua alma a comida deliciosa.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
Sua carne desaparece da vista, e seus ossos, que antes não se viam, aparecem.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
Sua alma se aproxima da cova, e sua vida dos que causam a morte.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
Se com ele, pois, houver algum anjo, algum intérprete; um dentre mil, para anunciar ao ser humano o que lhe é correto,
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
Então [Deus] terá misericórdia dele, e [lhe] dirá: Livra-o, para que não desça à perdição; [já] achei o resgate.
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Sua carne se rejuvenescerá mais do que era na infância, [e] voltará aos dias de sua juventude.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
Ele orará a Deus, que se agradará dele; e verá sua face com júbilo, porque ele restituirá ao ser humano sua justiça.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
Ele olhará para as pessoas, e dirá: Pequei, e perverti o [que era] correto, o que de nada me aproveitou.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
[Porém] Deus livrou minha alma para que eu não passasse à cova, e [agora] minha vida vê a luz!
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
Eis que Deus faz tudo isto duas [ou] três vezes com o ser humano,
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
Para desviar sua alma da perdição, e o iluminar com a luz dos viventes.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Presta atenção, Jó, e ouve-me; cala-te, e eu falarei.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
Se tiveres o que dizer, responde-me; fala, porque eu quero te justificar.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
E se não, escuta-me; cala-te, e eu ensinarei sabedoria.

< Ayubu 33 >