< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
C'est pourquoi, Job, écoute, je te prie, mon discours, et prête l'oreille à toutes mes paroles.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Voici maintenant, j'ouvre ma bouche, ma langue parle dans mon palais.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
Mes paroles [répondront à la] droiture de mon cœur, et mes lèvres prononceront une doctrine pure.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
L'esprit du [Dieu] Fort m'a fait, et le souffle du Tout-puissant m'a donné la vie.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
Si tu peux, réponds-moi, dresse-toi contre moi, demeure ferme.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Voici, je suis pour le [Dieu] Fort; selon que tu en as parlé; j'ai aussi été formé de la terre [tout comme toi].
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Voici, ma frayeur ne te troublera point, et ma main ne s'appesantira point sur toi.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
Quoi qu'il en soit, tu as dit, moi l'entendant, et j'ai ouï la voix de tes discours, [disant]:
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
Je suis pur, [et] sans péché; je suis net, et il n'y a point d'iniquité en moi.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Voici, il a cherché à rompre avec moi, il me tient pour son ennemi.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
Il a mis mes pieds aux ceps, il épie tous mes chemins.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
Voici, je te réponds qu'en cela tu n'as pas été juste; car Dieu sera toujours plus grand que l'homme [mortel].
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Pourquoi donc as-tu plaidé contre lui? car il ne rend pas compte de toutes ses actions.
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
Bien que le [Dieu] Fort parle une première fois, et une seconde fois à celui qui n'aura pas pris garde à la première;
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
Par des songes, par des visions de nuit, quand un profond sommeil tombe sur les hommes, et lorsqu'ils dorment dans leur lit;
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Alors il ouvre l'oreille aux hommes, et scelle leur châtiment.
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
Afin de détourner l'homme d'une [mauvaise] action, et de rabaisser la fierté de l'homme.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
[Ainsi] il garantit son âme de la fosse, et sa vie, de l'épée.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
L'homme est aussi châtié par des douleurs dans son lit, et tous ses os [sont brisés].
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
Alors sa vie lui fait avoir en horreur le pain, et son âme la viande désirable.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
Sa chair est tellement consumée qu'elle ne paraît plus; et ses os sont tellement brisés, qu'on n'y connaît plus rien.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
Son âme approche de la fosse, et sa vie, des choses qui font mourir.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
Que s'il y a pour cet homme-là un messager, qui parle pour lui, (un d'entre mille) qui manifeste à cet homme son devoir,
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
Alors il aura pitié de lui, et il dira: Garantis-le, afin qu'il ne descende pas dans la fosse; j'ai trouvé la propitiation.
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Sa chair deviendra plus délicate qu'elle n'était dans son enfance, et il sera rajeuni.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
Il fléchira Dieu par ses prières, et Dieu s'apaisera envers lui, et lui fera voir sa face avec joie, et lui rendra sa justice.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
Il regardera vers les hommes, et dira: J'avais péché, j'avais renversé le droit, et cela ne m'avait point profité.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
[Mais Dieu] a garanti mon âme, afin qu'elle ne passât point par la fosse, et ma vie voit la lumière.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
Voilà, le [Dieu] Fort fait toutes ces choses, deux [et] trois fois envers l'homme;
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
Pour retirer son âme de la fosse, afin qu'elle soit éclairée de la lumière des vivants.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Sois attentif, Job, écoute-moi; tais-toi, et je parlerai.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
Et si tu as de quoi parler, réponds-moi, parle; car je désire de te justifier.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
Sinon, écoute-moi, tais-toi, et je t'enseignerai la sagesse.

< Ayubu 33 >