< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
Cependant Job écoute mes paroles, prête une oreille attentive à ce que je vais dire.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Tu vois j'ouvre la bouche et ma langue se meut.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
La pureté de mon cœur se manifestera en mes discours; mes lèvres ne laisseront passer que des sentences irréprochables.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
L'esprit divin m'anime; le souffle du Tout-Puissant m'a instruit.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
Tu me répondras, si tu le peux; attends et tenons-nous face à face.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Je suis comme toi formé de boue; nous provenons du même Créateur.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Je ne veux ni me faire craindre, ni te troubler; ma main ne te sera pas pesante.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
Je n'ai rien perdu de ta défense, mes oreilles l'ont recueillie tout entière; tu as dit:
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
Je suis pur, je ne pèche point; je suis irréprochable, car j'observe les lois.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Dieu a trouvé sujet de m'accuser; il m'a jugé comme un ennemi.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
Il a mis mon pied dans une entrave; il a posé des sentinelles sur toutes mes voies.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
Comment as-tu osé dire: Je suis juste et Dieu ne m'a pas exaucé? L'Eternel n'est-il pas au-dessus de tous les humains?
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Tu as dit: Pourquoi Dieu n'a-t-il pas écouté un seul mot de ma cause?
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
Ce que le Seigneur a dit une fois, il le répète encore.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
En nos songes ou dans nos méditations nocturnes, à l'heure où les hommes assoupis sur leur couche ressentent une terreur surnaturelle,
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Il découvre leurs pensées; il donne une forme à leurs craintes secrètes; il les épouvante;
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
Il les détourne de l'iniquité; il préserve leur corps de la chute.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
A de tels humains, il a déjà sauvé la vie; il l'a empêché de succomber dans les batailles.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
Pour le blâmer derechef, il l'étend malade sur son lit; il engourdit tous ses os.
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
Et l'homme ne peut goûter d'aucun aliment; et son âme en désirera,
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
Jusqu'à ce que ses chairs pourrissent et que ses os vides de mœlle se montrent à nu.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
Son âme s'est approchée de la mort et sa vie de l'enfer. (questioned)
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
Mais, y eût-il là mille anges exterminateurs, pas un seul ne le blessera, si son cœur songe à se convertir à Dieu: le Seigneur lui fera connaître ce qu'il lui reproche; il lui montrera sa folie;
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
Il empêchera la mort de le saisir; il renouvellera son corps comme l'enduit d'un mur; il remplira ses os de mœlle;
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Il lui rendra des chairs délicates comme celles d'un enfant; il lui rendra sa virilité parmi les hommes.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
Ses prières au Seigneur seront exaucées; il verra le front serein, les manifestations de Dieu; il rendra justice à ses semblables.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
Alors il se fera des reproches en lui-même, disant: Qu'ai-je fait? Je n'ai point été puni comme le méritaient mes péchés.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
Mon Dieu, préservez mon âme d'entrer dans la perdition, et ma vie verra la lumière.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
Voilà donc ce que, de trois manières, le Tout-Puissant fait pour chacun des mortels.
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
C'est lui qui a protégé mon âme contre la mort, afin qu'à la lumière, ma vie chante ses louanges.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Prête l'oreille, Job; écoute-moi, garde le silence, c'est à moi seul de parler.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
Cependant, si tu as de bonnes raisons, réponds-moi; parle, je veux avec toi être juste;
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
Sinon, écoute; garde le silence et je t'instruirai.

< Ayubu 33 >