< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
“But now, Job, listen carefully to all that I am going to say [DOU].
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
I am ready to tell you [MTY, DOU] [what I think].
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
I know that I am speaking honestly and that I am speaking [MTY] sincerely.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
Almighty God has created me [as well as you], and his breath has caused me to live.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
So, answer [what] I [say] if you can; think carefully [about how you will reply to me].
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
“God considers that you, and I are both [equal]; he formed both of us from clay.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
So you do not need to be afraid of me; I will not crush/oppress you [by what I say] [MTY].
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
I have heard you [DOU] speaking, and this is what you have said:
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
‘I am innocent; I have not committed any sins; I am pure; I have not done things that are wrong.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
But God finds reasons to accuse me, and he considers that I am his enemy.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
[It is as though] he has put my feet (in stocks/between wooden blocks to prevent me from walking away), and he watches everything that I do.’ [MTY]
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
But what you have said is wrong, and I will tell you [what you have said that is wrong]. God is much greater than any human.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
So, (why are you arguing against God, saying ‘He never answers my questions’?/you should not be arguing against God, saying ‘He never answers my questions.’) [RHQ]
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
God does speak [to us] in various ways, but we do not pay any attention to what he says.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
[Sometimes he speaks to us] at night in dreams and visions, when we are on our beds, asleep [DOU].
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
He reveals things [MTY] to us and terrifies us by the things he warns us about.
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
He tell us those things in order that we stop doing [evil] things and to prevent us from becoming proud.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
He does not want us to be destroyed [MTY]; he wants to prevent us from dying [MTY] [while we are still young].
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
God also [sometimes] corrects us by forcing us to lie on our beds suffering much pain and with fever/aching in our bones.
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
The result is that we do not desire any food, not even very special food.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
Our bodies become very thin, with the result that we look like skeletons [HYP], and our bones stick out.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
[We know that] we will soon die and go to the place where dead people are.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
“But sometimes an angel [may come to one of us], one of the thousands of angels who come to intervene between us and God, to tell us what are the right things for us [to do].
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
The angel is kind to us and says to God, ‘Release that person, so that he does not descend to the place where dead people are! Do that because I have found the money to pay so that he can be released!
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Allow his body to be strong again; allow him to be strong like he was when he was a youth!’
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
When that happens, that person will pray to God, and God will accept/answer him; he will (enter God’s presence/worship God) joyfully, and then he will tell others how God saved him [from dying].
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
He will sing as he tells everyone, ‘I sinned, and I did things that were not right, but God did not punish me in the way that I deserved.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
He has saved me from dying and going to the place where dead people are, and I will continue to enjoy being alive.’
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
God does all these things for us many times;
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
he keeps us [SYN] from [dying and] going to the place where the dead are, in order that we can continue to enjoy being alive [IDM].
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
So Job, listen to me; do not say anything more; just allow me to speak.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
[After I speak], if you have something more that you want to say to me, say it, because I would like to find a way to declare that you (are innocent/have not done what is wrong).
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
But if you have nothing more that you want to say, then just listen to me, and I will teach you how to become wise.”

< Ayubu 33 >