< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
And but hear please O Job words my and all words my give ear to!
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Here! please I open mouth my it speaks tongue my on palate my.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
[are] [the] uprightness of Heart my words my and [the] knowledge of lips my purified they speak.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
[the] spirit of God it has made me and [the] breath of [the] Almighty it gives life me.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
If you will be able respond to me arrange! before me take your stand!
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Here! I [am] like mouth your to God from clay I was nipped off also I.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Here! dread of me not it will terrify you and pressure my on you not it will be heavy.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
Surely you have spoken in ears my and [the] sound of words I heard.
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
[am] pure I not transgression [am] innocent I and not iniquity [belongs] to me.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Here! occasions on me he finds he considers me to an enemy of him.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
He puts in the stock[s] feet my he watches all paths my.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
Here! this not you are in [the] right I will answer you for he is great God more than a human.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Why? against him have you contended that all words his not he answers.
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
For on one [occasion] he speaks God and on two [occasions] not anyone perceives it.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
In a dream - a vision of [the] night when falls deep sleep on people in slumber on a bed.
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Then he will uncover [the] ear of people and with discipline their he will seal.
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
To turn aside a person a deed and pride from a man he will cover.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
He will keep back life his from [the] pit and life his from passing away by missile.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
And he is chastened with pain on bed his (and [the] multitude of *Q(K)*) bones his [is] constant.
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
And it loathes it life his bread and self his food of desire.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
It wastes away flesh his from sight (and they are laid bare *Q(K)*) bones his [which] not they were seen.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
And it drew near to the pit self his and life his to [those who] bring death.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
If there on him - [is] an angel a mediator one of a thousand to tell to anyone uprightness his.
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
And he showed favor to him and he said deliver him from going down [the] pit I have found a ransom.
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
It grows fresh flesh his more than youth he returns to [the] days of youth his.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
He prays to God - and he accepted him and he saw face his with a shout of joy and he restored to a person righteousness his.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
He watches - over people and he said I have sinned and upright[ness] I have perverted and not it was equal to me.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
He has ransomed (self his *Q(K)*) from passing on in the pit (and life his *Q(K)*) on the light it will look.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
Here! all these [things] he does God two times three [times] with a man.
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
To bring back self his from [the] pit to be lighted up by [the] light of life.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Pay attention O Job listen to me keep quiet and I I will speak.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
If there [are] words respond to me speak for I desire to justify you.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
If not you listen to me keep quiet and I will teach you wisdom.

< Ayubu 33 >