< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
Now listen to me, Job. Pay attention to everything I have to say.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Look, I'm about to speak; my mouth is ready to talk.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
My words come from my upright heart; my lips speak sincerely of what I know.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
The spirit of God made me, and the breath of the Almighty gives me life.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
Answer me, if you can. Stand in front of me and prepare to defend yourself.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Look, before God we are both the same. I was also made from a piece of clay.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
See here, you don't need to be frightened of me. I won't be too hard on you.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
You spoke in my hearing and I have listened to everything you had to say.
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
You say, ‘I'm clean, I've done nothing wrong; I'm pure, I have not sinned.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
See how God finds fault with me and treats me as his enemy.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
He puts my feet in the stocks and watches everything I do.’
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
But look, you are wrong—let me explain. God is greater than any human being.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Why are you fighting against him, complaining that God isn't answering your questions?
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
God speaks over and over again, but people don't notice.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
Through dreams and visions in the night, when people fall into deep sleep, resting on their beds,
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
God speaks to them with solemn warnings
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
to turn them away from doing wrong and to stop them from becoming proud.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
He saves them from the grave and spares them from violent death.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
People are also disciplined on a bed of pain with constant aching in their bones.
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
They have no desire to eat; they do not even want their favorite dishes.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
Their flesh wastes away to nothing; all that's left is skin and bones.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
They are close to death; their lives approaching the executioner.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
But if an angel appears, a mediator, one of God's thousands of angels, to tell someone the right way for them,
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
he will be gracious to them. He will say, ‘Save them from going down into the grave, for I have found a way to free them.’
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Then their bodies will be renewed as if they were young again; they will be as strong as when they were in their prime.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
They will pray to God, and he will accept them; they come into God's presence with joy, and he will set things right for them.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
They sing, and tell others, ‘I sinned, I distorted what is right, but it did not do me any good.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
He saved me from going down into the grave and I will live in the light.’
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
Look, God does this time and again for people;
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
he saves them from the grave so they might see the light of life.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Pay attention Job, and listen to me! Be quiet—let me speak!
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
But if you have anything to say, then speak up.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
If not, listen to me. Keep quiet and I will teach you wisdom.”

< Ayubu 33 >