< Ayubu 33 >
1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
Howbeit, Job, I pray thee, hear mine utterances, and hearken to all my words.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Behold now, I have opened my mouth, my tongue speaketh in my palate,
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
My words shall be of the uprightness of my heart, and my lips shall utter knowledge purely.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
The Spirit of God hath made me, and the breath of the Almighty hath given me life.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
If thou canst, answer me; array [thy words] before me: take thy stand.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Behold, before God I am as thou; I also am formed out of the clay.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Behold, my terror shall not make thee afraid, nor my burden be heavy upon thee.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
Surely thou hast spoken in my hearing, and I have heard the voice of [thy] words: —
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
I am clean without transgression; I am pure, and there is no iniquity in me;
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Lo, he findeth occasions of hostility against me, he counteth me for his enemy;
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
He putteth my feet in the stocks, he marketh all my paths.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
Behold, I will answer thee in this, thou art not right; for God is greater than man.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Why dost thou strive against him? for he giveth not account of any of his matters.
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
For God speaketh once, and twice, — [and man] perceiveth it not —
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falleth upon men, in slumberings upon the bed;
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Then he openeth men's ears, and sealeth their instruction,
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
That he may withdraw man [from his] work, and hide pride from man.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
He keepeth back his soul from the pit, and his life from passing away by the sword.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
He is chastened also with pain upon his bed, and with constant strife in his bones;
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
And his life abhorreth bread, and his soul dainty food;
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
His flesh is consumed away from view, and his bones that were not seen stick out;
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
And his soul draweth near to the pit, and his life to the destroyers.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
If there be a messenger with him, an interpreter, one among a thousand, to shew unto man his duty;
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
Then he will be gracious unto him, and say, Deliver him from going down to the pit: I have found a ransom.
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
His flesh shall be fresher than in childhood; he shall return to the days of his youth.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
He shall pray unto God, and he will receive him with favour; and he shall see his face with shoutings, and he will render unto man his righteousness.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
He will sing before men, and say, I have sinned, and perverted what was right, and it hath not been requited to me;
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
He hath delivered my soul from going into the pit, and my life shall see the light.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
Lo, all these [things] worketh God twice, thrice, with man,
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
To bring back his soul from the pit, that he may be enlightened with the light of the living.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Mark well, Job, hearken unto me; be silent, and I will speak.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
If thou hast anything to say, answer me; speak, for I desire to justify thee.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
If not, hearken thou unto me; be silent, and I will teach thee wisdom.