< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
约伯啊,请听我的话, 留心听我一切的言语。
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
我现在开口, 用舌发言。
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
我的言语要发明心中所存的正直; 我所知道的,我嘴唇要诚实地说出。
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
神的灵造我; 全能者的气使我得生。
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
你若回答我, 就站起来,在我面前陈明。
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
我在 神面前与你一样, 也是用土造成。
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
我不用威严惊吓你, 也不用势力重压你。
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
你所说的,我听见了, 也听见你的言语,说:
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
我是清洁无过的,我是无辜的; 在我里面也没有罪孽。
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
神找机会攻击我, 以我为仇敌,
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
把我的脚上了木狗, 窥察我一切的道路。
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
我要回答你说:你这话无理, 因 神比世人更大。
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
你为何与他争论呢? 因他的事都不对人解说?
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
神说一次、两次, 世人却不理会。
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
人躺在床上沉睡的时候, 神就用梦和夜间的异象,
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
开通他们的耳朵, 将当受的教训印在他们心上,
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
好叫人不从自己的谋算, 不行骄傲的事,
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
拦阻人不陷于坑里, 不死在刀下。
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
人在床上被惩治, 骨头中不住地疼痛,
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
以致他的口厌弃食物, 心厌恶美味。
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
他的肉消瘦,不得再见; 先前不见的骨头都凸出来。
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
他的灵魂临近深坑; 他的生命近于灭命的。
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
一千天使中, 若有一个作传话的与 神同在, 指示人所当行的事,
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
神就给他开恩, 说:救赎他免得下坑; 我已经得了赎价。
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
他的肉要比孩童的肉更嫩; 他就返老还童。
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
他祷告 神, 神就喜悦他, 使他欢呼朝见 神的面; 神又看他为义。
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
他在人前歌唱说: 我犯了罪,颠倒是非, 这竟与我无益。
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
神救赎我的灵魂免入深坑; 我的生命也必见光。
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
神两次、三次向人行这一切的事,
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
为要从深坑救回人的灵魂, 使他被光照耀,与活人一样。
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
约伯啊,你当侧耳听我的话, 不要作声,等我讲说。
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
你若有话说,就可以回答我; 你只管说,因我愿以你为是。
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
若不然,你就听我说; 你不要作声,我便将智慧教训你。

< Ayubu 33 >