< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
Hateiteh Job, pahren lahoi ka dei e heh na thai pouh haw, ka lawk ka dei e heh na ngai pouh haw.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Atu ka pahni ka ang teh, ka pahni dawk hoi ka lai ni lawk a dei.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
Ka lawknaw heh kalan e ka lungthung hoi a tâco teh, ka pahni ni kathounge panuenae a pâpho.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
Cathut e Muitha ni na sak teh, Athakasaipounge kâha ni hringnae na poe.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
Na pathung thai pawiteh na pathung haw, ka hmalah na lawk hah bout kâpouk haw.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Atangcalah tetpawiteh, kai teh Cathut hmalah lawk ka dei pouh e lah ka o, kai hai vaiphu hoi sak e lah ka o van.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Kai dawk kaawm hoeh e takinae ni na takisak roeroe han, nahoeh pawiteh, ka kut heh na tak dawk ri poung mahoeh.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
Ka hnâthainae dawk na dei toung dawkvah, na lawk teh ka thai toe.
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
Na lawk ka ek hoeh dawkvah ka thoung, Yonnae ka tawn hoeh, payonpakainae kai dawk awm hoeh.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Hatei, kai taran nahane atueng kahawi a hmu teh, a taran patetlah na pouk.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
Ka khok hah hlong na buet teh, ka lamthung pueng hah a khet na ti.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
Khenhaw! hivah nang teh na lan hoeh, na pathung han, bangkongtetpawiteh, Cathut teh tami hlak a len.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Ama ni a lawk bangpatethai noutna mahoeh telah, bangkongmaw ama hah na pathoe.
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
Bangkongtetpawiteh, Cathut ni lam alouklah hoi lawk a dei thai, hatei, tami ni hmawt panuek hoeh.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
Karum a i navah vision dawk mat ka ip e, ikhun dawk a i lahun nah,
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Tami e hnâkâko hah a ang sak teh, amae cangkhainae hah a cak sak.
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
A sak e thung dawk hoi tami a ban teh, a kâoupnae dawk hoi hro lah ao thai nahanelah,
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
a hringnae hah tangkom thung hoi a kountouk teh, tahloi hoi duenae thung hoi a hringnae a rungngang.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
Tami teh a ikhun dawk patawnae hoi a yue teh, a hrunaw hah puenghoi patawnae hoi a pataw sak.
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
Hottelah a hringnae ni rawca a panuet teh, katuipounge rawca hai a hringnae ni a panuet.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
A takthai a kamsoe teh, kamnuek boihoeh e a hrunaw hah a kamnue.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
A hringnae ni tangkom hah a hnai teh, a hringnae ni kathetkung hah hoehoe a hnai.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
Ahni hanelah laiceinaw awm boipawiteh, kâponae kasakkung 1000 thung dawk tami buet tabang awm pawiteh, tami ni amae lannae hah a hmu sak thai nahanelah.
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
Ama ni tami hah a pahren teh, tangkom thung bonae koehoi ama teh a rungngang han, ratangnae buet touh ka hmu toe telah a ti.
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
A takthai teh camo e takthai patetlah bout ao vaiteh, a nawcanae patetlah bout ao han.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
Cathut koevah a ratoum vaiteh, ama teh a lathueng vah a lunghawi han, a minhmai hah lunghawi hoi a hmu han, bangkongtetpawiteh, ama ni tami teh a lannae hoi bout a ban sak.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
A huikonaw a khet teh ka yon toe, tamikalan hah ka rawp sak toe, hot teh kai hanelah banghai cungkeinae awmhoeh telah a ti.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
Tangkom thung e a hringnae hah a ratang vaiteh, a hringnae ni angnae a hmu han.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
Khenhaw! Cathut ni hete hnopueng heh, vai hni, atangcalah vai thum totouh tami koe a sak.
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
Hringnae angnae ni a ma hah a tue thai nahanelah, a hringnae tangkom thung hoi a tâco sak.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Na hnâpakeng nateh, Job na thai pouh haw, duem awm haw ka dei han.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
Dei hanelah na tawn pawiteh, na pathung haw, dei haw, bangkongtetpawiteh, yon ngaithoum hane na ngaikhai poung.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
Telah nahoeh pawiteh, na thai pouh haw, duem awm haw, lungangnae na dei pouh han.

< Ayubu 33 >