< Ayubu 32 >
1 Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
Así que estos tres hombres dejaron de responder a Job, porque era justo a sus ojos.
2 Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
Entonces se encendió la ira de Elihú, hijo de Baraquel, buzita, de la familia de Ram, contra Job. Su ira se encendió porque él se justificaba a sí mismo antes que a Dios.
3 Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
También se encendió su ira contra sus tres amigos, porque no habían encontrado respuesta, y sin embargo habían condenado a Job.
4 Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
Ahora bien, Elihú había esperado para hablar con Job, porque ellos eran mayores que él.
5 Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
Cuando Elihú vio que no había respuesta en la boca de estos tres hombres, se encendió su ira.
6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
Eliú, hijo de Baraquel, el buzita, respondió, “Yo soy joven, y tú eres muy viejo. Por eso me contuve y no me atreví a mostrarte mi opinión.
7 Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
Dije: “Los días deben hablar, y la multitud de años debe enseñar la sabiduría”.
8 Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
Pero hay un espíritu en el hombre, y el Espíritu del Todopoderoso les da entendimiento.
9 Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
No son los grandes los que son sabios, ni a los ancianos que entienden de justicia.
10 Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
Por eso le dije: “Escúchame; Yo también mostraré mi opinión”.
11 Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
“He aquí que he esperado tus palabras, y escuché su razonamiento, mientras buscabas qué decir.
12 Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
Sí, te he prestado toda mi atención, pero no hubo nadie que convenciera a Job, o que respondió a sus palabras, entre vosotros.
13 Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
Tened cuidado, no sea que digáis: “Hemos encontrado la sabiduría”. Dios puede refutarlo, no el hombre;’
14 Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
pues no ha dirigido sus palabras contra mí; tampoco le responderé con sus discursos.
15 Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
“Están asombrados. No responden más. No tienen nada que decir.
16 Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
¿Debo esperar, porque ellos no hablan, porque se quedan quietos y no responden más?
17 La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
Yo también responderé a mi parte, y también mostraré mi opinión.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
Porque estoy lleno de palabras. El espíritu dentro de mí me constriñe.
19 Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
He aquí que mi pecho es como el vino que no tiene salida; como los odres nuevos, está a punto de reventar.
20 Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
Voy a hablar para que me refresquen. Abriré mis labios y responderé.
21 Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
Por favor, no permitas que respete la persona de ningún hombre, ni daré títulos lisonjeros a ningún hombre.
22 Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.
Porque no sé dar títulos halagadores, o si no, mi Hacedor me llevaría pronto.