< Ayubu 32 >

1 Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
Omiserunt autem tres viri isti respondere Iob, eo quod iustus sibi videretur.
2 Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
Et iratus, indignatusque est Eliu filius Barachel Buzites, de cognatione Ram: iratus est autem adversum Iob, eo quod iustum se esse diceret coram Deo.
3 Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
Porro adversum amicos eius indignatus est, eo quod non invenissent responsionem rationabilem, sed tantummodo condemnassent Iob.
4 Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
Igitur Eliu expectavit Iob loquentem: eo quod seniores essent qui loquebantur.
5 Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
Cum autem vidisset quod tres respondere non potuissent, iratus est vehementer.
6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
Respondensque Eliu filius Barachel Buzites, dixit: Iunior sum tempore, vos autem antiquiores, idcirco demisso capite, veritus sum vobis indicare meam sententiam.
7 Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
Sperabam enim quod aetas prolixior loqueretur, et annorum multitudo doceret sapientiam.
8 Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
Sed, ut video, Spiritus est in hominibus, et inspiratio Omnipotentis dat intelligentiam.
9 Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
Non sunt longaevi sapientes, nec senes intelligunt iudicium.
10 Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
Ideo dicam: Audite me, ostendam vobis etiam ego meam sapientiam.
11 Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
Expectavi enim sermones vestros, audivi prudentiam vestram, donec disceptaremini sermonibus:
12 Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
Et donec putabam vos aliquid dicere, considerabam: sed, ut video, non est qui possit arguere Iob, et respondere ex vobis sermonibus eius.
13 Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
Ne forte dicatis: Invenimus sapientiam, Deus proiecit eum, non homo.
14 Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
Nihil locutus est mihi, et ego non secundum sermones vestros respondebo illi.
15 Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
Extimuerunt, nec responderunt ultra, abstuleruntque a se eloquia.
16 Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
Quoniam igitur expectavi, et non sunt locuti: steterunt, nec ultra responderunt:
17 La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
Respondebo et ego partem meam, et ostendam scientiam meam.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
Plenus sum enim sermonibus, et coarctat me spiritus uteri mei.
19 Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
En venter meus quasi mustum absque spiraculo, quod lagunculas novas disrumpit.
20 Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
Loquar, et respirabo paululum: aperiam labia mea, et respondebo.
21 Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
Non accipiam personam viri, et Deum homini non aequabo.
22 Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.
Nescio enim quamdiu subsistam, et si post modicum tollat me Factor meus.

< Ayubu 32 >