< Ayubu 32 >

1 Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
quei tre uomini cessarono di rispondere a Giobbe, perchè egli si riteneva giusto.
2 Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
Allora si accese lo sdegno di Eliu, figlio di Barachele il Buzita, della tribù di Ram. Si accese di sdegno contro Giobbe, perché pretendeva d'aver ragione di fronte a Dio;
3 Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
si accese di sdegno anche contro i suoi tre amici, perché non avevano trovato di che rispondere, sebbene avessero dichiarato Giobbe colpevole.
4 Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
Però Eliu aveva aspettato, mentre essi parlavano con Giobbe, perché erano più vecchi di lui in età.
5 Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
Quando dunque vide che sulla bocca di questi tre uomini non vi era più alcuna risposta, Eliu si accese di sdegno.
6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
Giovane io sono di anni e voi siete gia canuti; per questo ho esitato per rispetto a manifestare a voi il mio sapere. Presa dunque la parola, Eliu, figlio di Barachele il Buzita, disse:
7 Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
Pensavo: Parlerà l'età e i canuti insegneranno la sapienza.
8 Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
Ma certo essa è un soffio nell'uomo; l'ispirazione dell'Onnipotente lo fa intelligente.
9 Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
Non sono i molti anni a dar la sapienza, né sempre i vecchi distinguono ciò che è giusto.
10 Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
Per questo io oso dire: Ascoltatemi; anch'io esporrò il mio sapere.
11 Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
Ecco, ho atteso le vostre parole, ho teso l'orecchio ai vostri argomenti. Finché andavate in cerca di argomenti
12 Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
su di voi fissai l'attenzione. Ma ecco, nessuno ha potuto convincere Giobbe, nessuno tra di voi risponde ai suoi detti.
13 Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
Non dite: Noi abbiamo trovato la sapienza, ma lo confuti Dio, non l'uomo!
14 Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
Egli non mi ha rivolto parole, e io non gli risponderò con le vostre parole.
15 Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
Sono vinti, non rispondono più, mancano loro le parole.
16 Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
Ho atteso, ma poiché non parlano più, poiché stanno lì senza risposta,
17 La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
voglio anch'io dire la mia parte, anch'io esporrò il mio parere;
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
mi sento infatti pieno di parole, mi preme lo spirito che è dentro di me.
19 Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
Ecco, dentro di me c'è come vino senza sfogo, come vino che squarcia gli otri nuovi.
20 Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
Parlerò e mi sfogherò, aprirò le labbra e risponderò.
21 Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
Non guarderò in faccia ad alcuno, non adulerò nessuno,
22 Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.
perché io non so adulare: altrimenti il mio creatore in breve mi eliminerebbe.

< Ayubu 32 >