< Ayubu 32 >
1 Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
So had these three men abstained from answering Job; because he was righteous in his own eyes.
2 Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
Thereupon was kindled the wrath of Elihu the son of Barachel the Buzite, of the family of Ram: against Job was his wrath kindled, because he had declared himself more righteous than God.
3 Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
And against his three friends was his wrath kindled; because they had found no answer, and yet had condemned Job.
4 Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
Now Elihu had held back toward Job [his] words; because the others were older in days than he.
5 Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
But when Elihu saw that there was no answer in the mouth of these three men, then was his wrath kindled.
6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
And Elihu the son of Barachel the Buzite commenced, and said, Young am I in days, and ye are very old: therefore I hesitated and feared to show you what I know.
7 Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
I had said, Days shall speak, and multitude of years shall make wisdom known.
8 Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
But it is the spirit in man, and the breath of the Almighty which giveth them understanding.
9 Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
Not those rich in years must be always wise: neither do the aged constantly understand what is just.
10 Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
Therefore do I say, Hearken to me: I also will show forth what I know myself.
11 Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
Behold, I waited for your words: I gave an attentive ear to your reasonings, till you might have searched out the [proper] words.
12 Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
And now I understand you fully, and, behold, there is none that convinceth Job, or, that answereth his speeches among you.
13 Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
Say then not, We have found wisdom: God will thrust him down, not man.
14 Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
But he hath not directed any words against me: and with your speeches will I not answer him.
15 Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
They are dismayed, they answer no more: words have escaped away from them.
16 Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
And should I wait [longer], because they cannot speak, because they stand stilt and answer no more?
17 La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
[But] I also will surely answer my part, I myself also will show forth what I know;
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
For I am full of words, the spirit in my bosom urgeth me hard.
19 Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
Behold, my bosom is like [fresh] wine which hath not been opened: like new bottles it is ready to burst.
20 Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
I will speak, that I may breathe freer: I will open my lips and answer.
21 Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
On no account will I show undue favor to any man, and to no son of earth will I give flattering titles.
22 Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.
For I know not to give flattering titles; [for else] my Maker would speedily carry me away.