< Ayubu 32 >

1 Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
So these three men ceased to answer Job, because he was righteous in his own eyes.
2 Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
Then was kindled the wrath of Elihu the son of Barachel the Buzite, of the kindred of Ram: against Job was his wrath kindled, because he justified himself rather than God.
3 Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
Also against his three friends was his wrath kindled, because they had found no answer, and yet had condemned Job.
4 Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
Now Elihu had waited till Job had spoken, because they were elder than he.
5 Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
When Elihu saw that there was no answer in the mouth of these three men, then his wrath was kindled.
6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
And Elihu the son of Barachel the Buzite answered and said, I am young, and you are very old; why I was afraid, and dared not show you my opinion.
7 Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
I said, Days should speak, and multitude of years should teach wisdom.
8 Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
But there is a spirit in man: and the inspiration of the Almighty gives them understanding.
9 Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
Great men are not always wise: neither do the aged understand judgment.
10 Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
Therefore I said, Listen to me; I also will show my opinion.
11 Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
Behold, I waited for your words; I gave ear to your reasons, whilst you searched out what to say.
12 Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
Yes, I attended to you, and, behold, there was none of you that convinced Job, or that answered his words:
13 Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
Lest you should say, We have found out wisdom: God thrusts him down, not man.
14 Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
Now he has not directed his words against me: neither will I answer him with your speeches.
15 Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
They were amazed, they answered no more: they left off speaking.
16 Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
When I had waited, (for they spoke not, but stood still, and answered no more; )
17 La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
I said, I will answer also my part, I also will show my opinion.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
For I am full of matter, the spirit within me constrains me.
19 Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
Behold, my belly is as wine which has no vent; it is ready to burst like new bottles.
20 Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
I will speak, that I may be refreshed: I will open my lips and answer.
21 Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
Let me not, I pray you, accept any man’s person, neither let me give flattering titles to man.
22 Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.
For I know not to give flattering titles; in so doing my maker would soon take me away.

< Ayubu 32 >