< Ayubu 32 >

1 Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
But these three men ceased to answer Job, because he considered himself justified.
2 Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
And Eliu the son of Barachel the Buzite, of the kindred of Ram, was angry and indignant. But he was angry against Job because he described himself to be just in the presence of God.
3 Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
Moreover, he was indignant with his friends because they had not found a reasonable response, except in so far as they condemned Job.
4 Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
Therefore, Eliu waited while Job was talking, for these were his elders that were speaking.
5 Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
But when he saw that these three were not able to respond, he was extremely angry.
6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
And so Eliu the son of Barachel the Buzite responded by saying: I am younger in years, and you are more ancient; therefore, I kept my head low, for I was afraid to reveal to you my opinion.
7 Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
For I had hoped that greater age would speak, and that a multitude of years would teach wisdom.
8 Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
But I see now that there is only breath in men, and that it is the inspiration of the Almighty that gives understanding.
9 Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
The wise are not the aged, nor do the elders understand judgment.
10 Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
Therefore, I will speak. Listen to me, and so I will show you my wisdom.
11 Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
For I have endured your words; I have paid attention to your deliberations, while you were being argumentative with words.
12 Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
And as long as I supposed that you were saying something, I considered; but now I see that there is none of you that is able to argue with Job and to respond to his words.
13 Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
So that you will not say, “We have found wisdom,” God has thrown him down, not man.
14 Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
He has said nothing to me, and I will not respond to him according to your words.
15 Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
Then they were filled with dread, and so they no longer responded, and they withdrew from their speechmaking.
16 Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
Therefore, because I have waited and they have not been speaking, for they stood firm and did not respond at all,
17 La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
I also will answer in my turn, and I will reveal my knowledge.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
For I am full of words, and the feeling in my gut inspires me.
19 Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
Yes, my stomach is like fermenting wine without a vent, which bursts the new containers.
20 Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
I should speak, but I will also breathe a little; I will open my lips, and I will answer.
21 Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
I will not esteem the reputation of a man, and I will not equate God with man.
22 Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.
For I do not know how long I will continue, and whether, after a while, my Maker might take me away.

< Ayubu 32 >