< Ayubu 32 >
1 Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
So these three men gave no more answers to Job, because he seemed to himself to be right.
2 Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
And Elihu, the son of Barachel the Buzite, of the family of Ram, was angry, burning with wrath against Job, because he seemed to himself more right than God;
3 Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
And he was angry with his three friends, because they had been unable to give him an answer, and had not made Job's sin clear.
4 Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
Now Elihu had kept quiet while Job was talking, because they were older than he;
5 Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
And when Elihu saw that there was no answer in the mouth of the three men, he was very angry.
6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
And Elihu, the son of Barachel the Buzite, made answer and said, I am young, and you are very old, so I was in fear, and kept myself from putting my knowledge before you.
7 Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
I said to myself, It is right for the old to say what is in their minds, and for those who are far on in years to give out wisdom.
8 Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
But truly it is the spirit in man, even the breath of the Ruler of all, which gives them knowledge.
9 Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
It is not the old who are wise, and those who are full of years have not the knowledge of what is right.
10 Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
So I say, Give ear to me, and I will put forward my knowledge.
11 Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
I was waiting for your words, I was giving ear to your wise sayings; while you were searching out what to say,
12 Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
I was taking note; and truly not one of you was able to make clear Job's error, or to give an answer to his words.
13 Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
Take care that you do not say, Wisdom is here; God may overcome him, but not man.
14 Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
I will not put forward words like these, or make use of your sayings in answer to him.
15 Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
Fear has overcome them, they have no more answers to give; they have come to an end of words.
16 Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
And am I to go on waiting while they have nothing to say? while they keep quiet and give no more answers?
17 La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
I will give my answer; I will put forward my knowledge:
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
For I am full of words, I am unable to keep in my breath any longer:
19 Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
My stomach is like wine which is unable to get out; like skins full of new wine, it is almost burst.
20 Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
Let me say what is in my mind, so that I may get comfort; let me give answer with open mouth.
21 Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
Let me not give respect to any man, or give names of honour to any living.
22 Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.
For I am not able to give names of honour to any man; and if I did, my Maker would quickly take me away.